Featured
Showing posts with label Local News. Show all posts
Showing posts with label Local News. Show all posts

Thursday, May 25, 2017

RC Shinyanga azuiwa kuingia mgodini



Msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Tellack, umezuiwa kuingia katika mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu alikokwenda kukagua iwapo uzalishaji unaendelea bila kuwepo kwa Maofisa wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini, TMAA.

Maofisa wa TMAA waliondoka mara baada ya ripoti ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu kukabidhiwa kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli hapo jana ikulu jijini Dar es sallaam.

Bi. Zainabu amesema ameagiza Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi katika eneo lote la mgodi huo kuhakikisha hakuna mtu anayetoka wala kuingia

Mapema leo Mkuu huyo wa Mkoa alitembelea mgodi mwingine wa Buzwagi ambao pia unamilikiwa na kampuni ya Acacia kama ulivyo ule wa Bulyanhulu.

Katika mgodi wa Buzwagi, Bi. Zainab na msafara wake waliruhusiwa kuingia na kushuhudia shughuli za uchimbaji zikiwa zimesitishwa kwa kukosekana maofisa wa TMAA walioondoka mara baada ya Rais Magufuli kutangaza kuvunja bodi na kutengua uteuzi wa watendaji wakuu wa wakala hiyo.

Saturday, February 11, 2017

Mabalozi wafunguka kinachowakuna kwa JPM



Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania, wamempongeza Rais Magufuli pamoja na serikali ya awamu ya tano kwa jitihada zake za kupambana na rushwa, kujenga nidhamu kwa watumishi wa umma na kuimarisha uchumi.
Akizungumza kwa niaba ya mabalozi wenzake katika sherehe ya kuaga mwaka mpya kwa Mabalozi na Wawakilishi wa mashirika ya kimataifa (New Year Diplomatic Sherry Party) iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, Kiongozi wa wanadiplomasia hao Mhe. Edzai Chimoyo ambaye ni Balozi wa Zimbabwe hapa nchini, ameahidi kuwa yeye na wenzake wapo tayari kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Awamu ya Tano.
Pia amepongeza juhudi kubwa zilizofanywa kufufua Shirika la Ndege (ATCL) kwa kununua ndege mpya ambazo licha ya kurahisisha usafiri zitasaidia kukuza sekta ya utalii hapa nchini.
Akihutubia sherehe hizo, Rais John Magufuli amezialika nchi mbalimbali na wadau mbalimbali wa maendeleo kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kujenga uchumi wa viwanda utakaoiwezesha Tanzania kuingia katika nchi ya kipato cha kati.

Mhe. Dkt. Magufuli amesema ifikapo mwaka 2020 Tanzania imedhamiria uchumi wake ukue kwa wastani wa asilimia 10, sekta ya Viwanda iajiri asilimia 40 ya watanzania na pato la mtu kwa mwaka likue hadi kufikia wastani wa Dola 3,000 za kimarekani (sawa na Shilingi na takribani shilingi Milioni 6 na Laki 6 kwa mwaka)

Pia amewaomba wawahamasishe wadau watakaokuwa tayari kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi ikiwemo ujenzi wa reli ya kati yenye urefu wa Kilometa 1,200 kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge)kuanzia Dar es Salaam hadi Mwanza na Kigoma na kuunganisha hadi nchi za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda,na kwamba tayari Serikali itaanza kujenga Kilometa 300 za kuanzia Dar es Salaam mwaka huu.
Kuhusu mwaka uliopita, Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali imeanza kutekeleza awamu ya pili ya Mpango wa Maendeleo (2016-2021) uliopangwa kugharimu Shilingi Trilioni 107 ambapo kati ya fedha hizo Shilingi Trilioni 59 zitatolewa na Serikali ya Tanzania na kiasi kinachobaki kitatolewa na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Mhe. Dkt. Magufuli amebainisha kuwa katika kutekeleza mpango huo, Serikali imechukua hatua ya kuongeza bajeti ya maendeleo kutoka asilimia 26 hadi kufikia asilimia 40 katika mwaka huu.

Saturday, January 21, 2017

China yafungua Milango kwa vijana wa kitanzania


Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Augustino Mahiga amesema China imekubali kutoa fursa za masomo nchini mwao kwa vijana wa Tanzania ambao ndiyo watapewa kipaombele cha ajira katika viwanda vitakavyowekezwa na nchi hiyo hapa nchini
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali ya Tanzania na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu Youqing baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam.Maadhimisho hayo yanafanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuanzia saa 4;00 asubuhi hadi saa 11 jioni na yanatarajiwa kumalizika kesho tarehe 22 Januari 2017.

Akizungumza jijini Dar es salaam leo katika sherehe za maadhimisho ya mwaka mpya wa Kichina unaofahamika kama 'Jogoo', Balozi Mahiga amesema ni wakati sasa kwa watanzania kuchangamkia fursa hiyo ya masomo ili kupata ajira nyingi za watanzania.
Kwa upande wake waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji akizungumza katika sherehe hizo Charles Mwijage amesema kuna miradi mingi ya uwekezaji ya China ambayo itawekezwa hapa nchini ikiwemo bandari na viwanda vitakavyoshughulika na teknolojia mbalimbali 

Thursday, January 12, 2017

Tazama picha Tano za meli kubwa AZAM SEA LINK ikiwasili Zanzibar




Meli kubwa zaidi  afrika mashari na ya kisas AZAM SEA LINK aina ya RORO iliwasili katika bandari ya Zanzibar jana tayari kwa kunza  safari zake kati ya Dar as Salaam na Zanzibar.


Meli hiyo yenye uwezo mkubwa wa kubeba abiria wapatao 1650,mizigo uzito wa tani 717,sambamba namagari 150  meli hii inatarjiwa kurahisiha zaidi mawasiliano kati ya pandezote mbili  na kuchochea shugulu za kiuchumi 

Mbunge Chadema atupwa jela miezi sita


Mahakama ya wilaya ya Kilombero imemuhukumu kifungo cha miezi sita jela Mbunge Wa jimbo la Kilombero Peter Lijualikali (30)   kwa kosa la kufanya fujo na kusababisha taharuki katika maeneo ya ukumbi Wa halmashauri ya Wilaya ya Kilombero
Mwendesha mashtaka inspekta Wa Polisi Dotto Ngimbwa aliiambia mahakama kuwa mshtakiwa, akiwa mshtakiwa namba moja pamoja na mwenzie Stephano Mgata (35) walitenda kosa hilo Machi mosi mwaka 2016 saa 4 asubuhi Kwenye kikao cha Baraza la Madiwani katika eneo la Kibaoni ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero.

Ngimbwa alisema washtakiwa hao kwa pamoja walifanya fujo kinyume na kifungu namba 89 kifungu kidogo cha kwanza B, cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002, ambapo washtakiwa walikana mashtaka na hivyo kufanya kesi kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili na upande wa mashtaka ukathibitisha shtaka bila kuacha shaka.

Hakimu mkazi katika mahakama ya wilaya ya Kilombero Timothy Lyon alisema mahakama imewatia hatiani kwa kosa hilo na kwa kuwa mshtakiwa Wa kwanza ni Mbunge ambaye alikuwa na kesi tatu huko nyuma na kutiwa hatiani amehukumuwa jela miezi sita.

Lyon alizitaja kesi za nyuma ambazo mbunge huyo alitiwa hatiani NA kuhukumiwa ni kesi namba 338 ya mwaka 2014, kesi namba 220 ya mwaka 2014 na kesi namba 340 ya mwaka 2014, hivyo kutokana na mshtakiwa ni mzoefu katika kesi zote, mahakama imemkuta na hatia ya kwenda jela miezi sita.
Moja kati ya matukio ya vurugu yaliyomuhusisha mbunge huyo, na hapa ilikuwa ni katika kikao cha uchaguzi wa mwenyekiti wa halmashauri
Hata hivyo mahakama hiyo imeona kwa kuwa mshtakiwa wa pili Stephano Mgata (35), hii ni Mara yake ya kwanza amehukumiwa kifungo cha miezi sita nje ambapo ndani ya kipindi hicho cha miezi sita hatotakiwa kutenda kosa lolote la jinai.
Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida hali katika mahakama hiyo ilikuwa tulivu tofauti na kesi nyingine dhidi ya Mbunge Lijualikali, ambapo wafuasi wachache wanaodhaniwa kuwa ni wa Chadema ndiyo walijitokeza na baada ya hukumu kutolewa Mbunge huyo alipelekwa haraka gerezani kwenda kuanza kutumikia kifungo chake
Kutokana na jambo hili mwanasiasa Julius Mtatiro anasema kuwa licha ya Lijualikali kufungwa jela lakini hali hiyo haiwezi kupoteza ubunge wake na kusema kama akikata rufaa huenda akapata haki. 

"Hawezi kupoteza ubunge kwa kifungo hicho na kama akikata rufaa anaweza kupata haki, Kumfunga Lijuakali kwa sababu alihoji na kupinga kunyimwa haki yake ni kuzalisha Lijualikali wengi zaidi" alisema Julius Mtatiro 

Tuesday, January 3, 2017

JPM aagiza kufutwa kwa utitiri wa kodi



Ikiwa Tanzania Inataraji Mpaka ifikapo waka 2020 iwekweyne uchumi wakati hivi leo Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Wakuu wa Mikoa,Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuondoa utitiri wa kodi uliopo kwenye Mazao ili wakulima waweze kunufaika kutokana na kujiongezea kipato.

Agizo hilo alimetolewa leo wakati akihutubia wakazi wa Wilaya ya Bukoba na watanzania kwa ujumla akiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Kagera.

“Nawaagiza Wakuu wa Mikoa,Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri kupitia upya Kodi zilizopo katika bidhaa mbalimbali kama Kahawa na Pamba, hakikisheni mnaondoa utitiri huu wa Kodi ili wafanyabiashara hawa wafaidike na mazao yao,” Alisema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amewaahidi watanzania kuwa atahakikisha anafanya kazi usiku na mchana bila kujali itikadi, dini na makabila ili kuhakikisha nchi inasonga mbele katika nyanja zote za kimaendeleo.
Akizungumzia maendeleo ya michango mbalimbali kwa ajili ya wathirika wa tetemeko la Ardhi mkoani Kagera Rais Magufuli amesema kuwa mpaka sasa simenti iliyochangwa ni zaidi ya tani 30,600 na mabati zaidi ya elfu 31,000 ambapo wananchi wameshaanza kupewa na kujengea.

Amewahimiza wananchi walioathirika na tetemeko la Ardhi kutotegemea Serikali kuwafanyia kila kitu na badala yake waanze kujenga na watumie msimu huu wa mvua kulima ili kujipatia chakula.
Pia Rais Magufuli amewashukuru na kuwapongeza wahisani waliochangia Maafa ya Kagera na kuwataka kuendelea na moyo huo katika kulijenga Taifa letu.  

Monday, January 2, 2017

Mkurugenzi wa TANESCO atumbuliwa na Rais Magufuli



Rais John Pombe Magufuli leo tarehe 1/1/ 2017 ametengua uteuzi  uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania 9TANESCO) Mhandisi Felchesmi Mramba na kumteua Dk Tito Esau Mwinuka kuwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo.

Akiwa mkoani Kagera leo Rais Magufuli alisikika akisema kuwa haiwezekani mtu mmoja kutokana na nafasi yake afanye maamuzi ya kupandisha umeme huku akitambua kuwa kufanya hivyo ni kuwaumiza watanzania na kuahidi kuendelea kuwatumbua wafanyakazi wa Serikali ambao ni majipu.
Kwa mwaka 2017 Mkurugenzi wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba anakuwa mfanyakazi wa kwanza kutumbuliwa na Rais John Pombe Magufuli

Tuesday, November 29, 2016

UTAFITI WA KWANZA WA CHANJO YA HIV YA ANZA KUSINI MWA AFRICA


Utafiti kuhusu ufanisi wa chanjo ya kwanza ya VVU waaanza huko Afrika Kusini! Je, una imani chanjo hiyo itatokomeza UKIMWI?


Taasisi ya Afya ya Marekani imesema, utafiti kuhusu ufanisi wa chanjo ya kwanza ya VVU utakaodumu kwa miaka saba umeanza nchini Afrika Kusini, ili kujaribu kama chanjo hiyo inaweza kutoa kinga yenye ufanisi dhidi ya virusi vya UKIMWI. Utafiti huo unalenga kuwashirikisha wanaume na wanawake 5,400 wenye umri wa miaka 18 hadi 35, na kuwa majaribio makubwa zaidi ya chanjo ya VVU nchini Afrika Kusini, ambako zaidi ya watu elfu 1 wanaambukizwa virusi hivyo kila siku.

Tumepata maendeleo mengi katika mapambano dhidi ya UKMWI, lakini bado hatujafanikiwa kutokomeza maambukizi ya ugonjwa huo. 

Je, Una imani kuwa sisi binadamu tunaushinda ugonjwa huo? Unadhani itachukua miaka mingapi kupata ushindi wa mwisho katika mapambano hayo dhidi ya UKIMWI?

Thursday, November 17, 2016

Rwand Air yakamilisha Ununua Ndenge Boeing 737-800 Next Gen


wakati tanzania ikinunua ndege  mbili aina ya Bombardier Dash 8 Q400  na Bombardier Dash 8 Q300 siku chache tu  zilizopita .Wenzao Shirika la ndege la Rwanda RwandAir limenunua ndege moja aina ya Boeing 737-800 Next Gen ikitarajia kuboresha ushindani wake katika safari za anga duniani .

RwandAir imekuwa ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kununua ndege ya aina hiyo ambayo imewekwa vifaa vya kuwezesha abiria kutumia huduma za intaneti kwa njia ya WiFi.
Ndege hiyo ina iuwezo wa kubeba abiria 154.
 
Waziri wa uchukuzi wa Rwanda Alexis Nzahabwanimana, amesema ndege hiyo mpya itawezesha shirika hilo kupanua safari zake barani Asia, Ulaya na Marekani.

SERIKALI YA TANZANIA YATOA MSIMAMO WAKE KUHUSU ICC



Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito kwa nchi wanachama wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC, kuendelea kuunga mkono uwepo wa chombo hicho wakati huu ambapo baadhi ya nchi zinaendelea kujitoa.

Akizungumza huko The Hague, Uholanzi kwenye mkutano wa nchi wanachama wa mkataba wa Roma ulionzisha ICC, Zeid amesema kujitoa kwa baadhi ya nchi kunaonekana kuwa na lengo la kulinda viongozi wao dhidi ya mashtaka.

Amesema anasikitishwa na hali ilivyo kwani nchi za Afrika zimekuwa msingi wa mahakama hiyo, lakini anatiwa moyo kuwa Botswana, Cote d'Ivoire, Nigeria, Malawi, Senegal, Tanzania, Zambia na Sierra Leone zimesema zitaendelea kuwa wanachama.

Zeid ametoa kauli hiyo wakati huu ambapo yaelezwa Urusi ina mpango wa kujitoa, wakati nchi tatu za Afrika; Burundi, Afrika Kusini na Gambia tayari zilishatangaza kujitoa

 Hii leo imeelezwa kuwa baadhi ya nchi zimesema zitaendelea kuwepo ndani ya chombo hicho cha haki, nazo ni Botswana, Cote d'Ivoire, Nigeria, Malawi, Senegal, Tanzania, Zambia na Sierra Leone.
Kamishna wa haki za binadamu Zeid Ra'ad al Hussein amepongeza hatua hiyo akisema chonde chonde jamani msitoke!

Wednesday, November 16, 2016

SERIKALI IMEPANIA KUBADILISHA UONGOZI WOTE WA ATCL


Tanzania inapanga kuufanyia mabadiliko uongozi wa Shirika lake la ndege
Tanzania imesema inapanga kuufanyia mabadiliko uongozi wa shirika lake la ndege ili libaki na wafanyakazi bora, na kuboresha utendaji wa shirika hilo.

Waziri wa ujenzi, usafirishaji na mawasiliano wa Tanzania Prof Makame Mbarawa, amesema ili shirika hilo liweze kuhimili ushindani wa kikanda linatakiwa kuboresha utendaji wake.

Amesema serikali ya awamu ya tano ina nia thabiti ya kuboresha shirika hilo na kuwa moja ya mashirika mazuri kwenye eneo la Afrika Mashariki ndani ya miaka mitano. Kwanza ameupa uongozi wa juu wa shirika hilo muda wa mwezi mmoja kufanya mabadiliko ili kubaki na wafanyakazi wenye uwezo.

Hivi karibuni serikali ya Tanzania iliagiza ndege mbili za abiria, na imepanga kuagiza ndege mbili zaidi, na kuhakikisha kuwa kabla ya mwaka 2018 inakuwa na ndege saba.

Monday, October 31, 2016

UNESCO wajenga kituo cha kumbukumbu za jamii ya KIMASAI

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni – UNESCO, kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya –EU- wamejenga kituo cha utamaduni kitakachotumika kutunza kumbukumbu muhimu za jamii ya kimasai na kutoa elimu za kitamaduni kwa njia ya kieletroniki katika wilaya ya NGORONGORO mkoani ARUSHA.
Mwakilishi wa UNESCO nchini, ANNA CONSTANTINE, amesema kituo hicho kitasaidia kutoa elimu mbali mbali hasa kuhusu namna ya kuhifadhi tamaduni
Kwa upande wake Mwakilishi toka Umoja wa Ulaya- EU-OLIVIER COUPLEX,  amesema makubaliano yakuanza ujenzi wa mradi huo wa kituo cha utamaduni ulifikiwa mwaka 2012 baina ya serikali ya TANZANIA na Umoja wa Ulaya EU.

Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akimwelezea Katibu Tawala, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Lemuel Kristian Kileo (wa pili kushoto), namna mradi wa ujenzi wa kituo cha sanaa.


Mkuu wa mkoa wa ARUSHA, MRISHO GAMBO, amelishukuru shirika la UNESCO pamoja na Umoja wa ulaya EU kwa jitihada mbali mbali za kuleta maendeleo nchini na pia amesema kituo hicho  kitasaidia kutunza kumbukumbu muhimu kuhusu tamaduni za maasai kutokana na jamii hiyo kuwa na tamaduni nyingi ambazo zimekuwa kivutio kikubwa ndani na nje ya nchi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni – UNESCO, kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya –EU- wamejenga kituo cha utamaduni kitakachotumika kutunza kumbukumbu muhimu za jamii ya kimasai na kutoa elimu za kitamaduni kwa njia ya kieletroniki katika wilaya ya NGORONGORO mkoani ARUSHA.
Mwakilishi wa UNESCO nchini, ANNA CONSTANTINE, amesema kituo hicho kitasaidia kutoa elimu mbali mbali hasa kuhusu namna ya kuhifadhi tamaduni
Kwa upande wake Mwakilishi toka Umoja wa Ulaya- EU-OLIVIER COUPLEX,  amesema makubaliano yakuanza ujenzi wa mradi huo wa kituo cha utamaduni ulifikiwa mwaka 2012 baina ya serikali ya TANZANIA na Umoja wa Ulaya EU.

Mkuu wa mkoa wa ARUSHA, MRISHO GAMBO, amelishukuru shirika la UNESCO pamoja na Umoja wa ulaya EU kwa jitihada mbali mbali za kuleta maendeleo nchini na pia amesema kituo hicho  kitasaidia kutunza kumbukumbu muhimu kuhusu tamaduni za maasai kutokana na jamii hiyo kuwa na tamaduni nyingi ambazo zimekuwa kivutio kikubwa ndani na nje ya nchi.

Sunday, October 30, 2016

Watu Wawili wahukumiwa kifo kutokana na mauaji ya binti mwenye ualbino



Mahakama kuu kanda ya BUKOBA imetoa hukumu ya kunyongwa hadi kufa kwa LAMECK BAZIL na PANCRAS MINAGO baada ya kupatikana na hatia ya kula njama na kumuua kwa kukusudia marehemu  MAGDALENA ANDREA ambaye alikuwa na ualbino.

Watu hao walifanya kosa hilo mwaka 2008 katika wilaya ya BIHARAMULO Mkoani KAGERA na hukumu ya kesi hiyo namba 57 ya mwaka 2015 inaweka rekodi kwa kuwa kesi ya kwanza katika mahakama kuu kanda ya BUKOBA kutoa  adhabu ya kifo dhidi ya watu waliotenda kosa la mauaji kwa watu wenye ualbino.


Mnamo Septemba 21 mwaka 2008 katika kijiji cha LUSABYA katika kata ya RUNAZI wilayani BIHARAMULO Mkoani KAGERA, LAMECK BAZIL ambaye ni mganga wa jadi mwenyeji wa mkoa wa MARA ambaye alifika kijijini hapo kwa shughuli za utabibu alimshawishi baba mkwe wake PANCRAS MINAGO kumshambulia na kisha kumuua  MAGDALENA ANDREA kwa lengo la kunyofoa baadhi ya viungo vyake ili kwenda kuviuza.

MACHINGA watakiwa kuondoka maeneo yasiyo rasmi


Mkuu wa mkoa wa DAR ES SALAAM, - PAUL MAKONDA ametoa muda siku 14 kwa wakuu wote wa wilaya za mkoa huo kuandaa maeneo

Mkuu wa mkoa wa DAR ES SALAAM, - PAUL MAKONDA ametoa  muda siku 14  kwa wakuu wote wa wilaya za mkoa huo kuandaa maeneo ya kufanyiabiashara   kwa wafanyabiashara wadogo maarufu kama MACHINGA.
Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini DAR ES SALAAM, - MAKONDA  amepiga marufuku wafanyabiashara hao kufanya shughuli zao maeneo yasiyo rasmi.
MAKONDA amesema kuwa wafanyabiashara hao wadogo  wanatakiwa kufanya biashara  zao katika  maeneo rasmi na si kando ya barabara na  pembezoni mwa maduka, na pia amewataka kuacha kutumia  vibaya ruhusa ya Rais JOHN MAGUFULI aliyetaka kutobughudhiwa kwa Wafanyabiashara hao wadogo


Bodi ya mikopo Imesisitiza kufanya uhakiki wa wanafunzi.......




Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu(HESLB) imesema itaanza uhakiki wa taarifa za wanafunzi wanufaika wanaoendelea na masomo ili kujiridhisha kama wanasifa sitahiki na ambao watakuta hawana sifa watasitishiwa mkopo.
Mkurugenzi wa mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema zoezi hilo litaanza Jumanne na wanafunzi wote watatakiwa kujaza dodoso ambalo litatolewa ambalo litawekwa kwenye mtandao wa bodi hiyo.

Thursday, October 6, 2016

Zanzibar kufanyia mabadiliko katiba


Serikali ya Zanzibar imefanyia mabadiliko katiba ili kutoa uwezo kwa Rais wa Zanzibar kuteua wajumbe wa Tume ya Uchaguzi bila kushauriana na kiongozi wa kambi ya upinzani ndani ya baraza la wawakilishi.

Saturday, September 24, 2016

BARUA KUTOKA SAUDI ARABIA,BAKWATA HUENDA IKAFUNGIWA KUPELEKA MAHUJAJI..


Friday, September 23, 2016

Mauaji ya Watu Weusi Yaendelea Katika Mji wa Marekani


Gavana wa jimbo la North Carolina ametangaza hali ya hatari katika mji wa Charlotte, wakati ghasia zinaendelea kufuatia polisi kumuua mwanamume mweusi.
Ghasia zilizuka kwa usiku wa pili baada ya kuuawa Keith Lamont Scott kwa kupigwa risasi na afisa mweusi Jumanne.
Muandamanaji mmoja yupo katika hali mahututi baada ya kuzuka ufyetulianaji risasi baina ya raia, maafisa wa mji walisema.
Bwana Scott was ni mwanamume wa tatu raia wa Marekani mwenye asili ya kiafrika kuuawa na polisi katika wiki moja.
Mauaji haya yamesbabisha maandamano makubwa katika siku za hivi karibuni



Polisi ya kupmabana na fujo imetumia gesi ya kutoa machozi walipokabiliana na mamia ya waandamanj. Idara ya polisi inasema maafisa wake wanne wamejeruhiwa.
Awali Gavana wa North Carolina Governor Pat McCrory amesema ameanzisha jitihada kutuma jeshi la ulinzi na maafisa wa polisi wa trafiki kusaidia kukabiliana na maandamano hayo.
"ghasia zozote zinazoelekezwa dhidi ya raia wetu au maafisa wa polisi au kusababisha uharibifu wa mali hazikubaliki," alisema.
Waandamanji wana hasira kuwa bwana Scott, mwenye umri wa miaka 43, ameuawa na Polisi Jumanne mchana katika hali ya kutatanisha karibu na eneo la makaazi.

Monday, August 29, 2016

Break news Kikao Cha Ndani Cha Kamati Kuu ya Chadema Chavamiwa na Polisi....



DAR: Kikao cha ndani cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichokuwa kinaendelea katika Hoteli ya Giraffe eneo la Mbezi kimevamiwa na Polisi.
- Sababu za kuvamiwa bado hazijajulikanahttp

Sunday, August 28, 2016

Waziri Simbachawene Aagiza Machinga waondolewe Kariakoo....Asema Rais hakumaanisha warudi.Fahamu zaidi hapa.




Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuwaondoa wafanyabiashara wadogo maarufu kama Machinga katika maeneo ya soko la Kariakoo na barabarani, hususan karibu na barabara za mabasi ya mwendo kasi.


Akizungumza jana na Kamati ya Bunge, Waziri huyo wa TAMISEMI alisema kuwa kurejea kwa wafanyabiashara hao katika maeneo hayo kumeleta usumbufu mkubwa na uchafu wa mazingira katika maeneo ya jiji.

“Namuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam awaondoe na asilegeze kamba,” alisema Waziri Simbachawene.

Alisema kuwa hali hiyo imetokana na tafsiri isiyo sahihi ya agizo la Rais John Magufuli alipokuwa ziarani Mkoani Mwanza.

“Wala agizo  la Mheshimiwa Rais halikumaanisha hicho. Mheshimiwa Rais alisema tuwatafutie maeneo mbadala ambao wapo maeneo kama ya Mwanza na walikuwa wanafanya biashara ya kuuza nguo, akizungumzia wale particular group walioko pale Mwanza. Kwa Dar es Salaam tulishamaliza huko,” alisema.

Aidha, alimtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhakikisha hakuna hata machinga mmoja atakayeonekana akifanya biashara katika maeneo ya barabara za mabasi yaendayo kasi.


Aigizo hilo la Waziri Simbachawene liliungwa Mkono na wajumbe wa Kamati hiyo ya Bunge ambao walisema kuwa hali ya soko la Kariakoo imekuwa mbaya kutokana na kuzagaa kwa machinga.
Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com