Monday, January 2, 2017

Mkurugenzi wa TANESCO atumbuliwa na Rais Magufuli



Rais John Pombe Magufuli leo tarehe 1/1/ 2017 ametengua uteuzi  uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania 9TANESCO) Mhandisi Felchesmi Mramba na kumteua Dk Tito Esau Mwinuka kuwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika hilo.

Akiwa mkoani Kagera leo Rais Magufuli alisikika akisema kuwa haiwezekani mtu mmoja kutokana na nafasi yake afanye maamuzi ya kupandisha umeme huku akitambua kuwa kufanya hivyo ni kuwaumiza watanzania na kuahidi kuendelea kuwatumbua wafanyakazi wa Serikali ambao ni majipu.
Kwa mwaka 2017 Mkurugenzi wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba anakuwa mfanyakazi wa kwanza kutumbuliwa na Rais John Pombe Magufuli

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com