Thursday, May 25, 2017

RC Shinyanga azuiwa kuingia mgodini



Msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Tellack, umezuiwa kuingia katika mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu alikokwenda kukagua iwapo uzalishaji unaendelea bila kuwepo kwa Maofisa wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini, TMAA.

Maofisa wa TMAA waliondoka mara baada ya ripoti ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu kukabidhiwa kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli hapo jana ikulu jijini Dar es sallaam.

Bi. Zainabu amesema ameagiza Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi katika eneo lote la mgodi huo kuhakikisha hakuna mtu anayetoka wala kuingia

Mapema leo Mkuu huyo wa Mkoa alitembelea mgodi mwingine wa Buzwagi ambao pia unamilikiwa na kampuni ya Acacia kama ulivyo ule wa Bulyanhulu.

Katika mgodi wa Buzwagi, Bi. Zainab na msafara wake waliruhusiwa kuingia na kushuhudia shughuli za uchimbaji zikiwa zimesitishwa kwa kukosekana maofisa wa TMAA walioondoka mara baada ya Rais Magufuli kutangaza kuvunja bodi na kutengua uteuzi wa watendaji wakuu wa wakala hiyo.

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com