Featured

Thursday, May 25, 2017

SportPesa Super Cup Kuieleta Timu ya Everton Bongo




Najua inawezekana ukawa na shauku ya kuona michuano ya SportPesa Super Cup inafanyika mapema zaidi kutokana na upendo wako na soka baada ya kusikia kuwa kampuni ya michezo ya kubashiri ya Sport Pesa imeanzisha mashindano hayo na yataanza June 5 hadi June 11 2017.
Good news nyingine iliyoritipotiwa leo na moja kati ya mitandao mikubwa England ni kuhusiana na club ya Everton kuwa itakuja Tanzania na Alhamisi ya July 13 itacheza mchezo mmoja wa kirafiki na moja kati ya timu nane zitakazoshiriki michuano ya SportPesa Super Cup.





Mtandao wa liverpoolecho.co.uk ndio umeripoti taarifa hizi huku ikithibitisha kuwa timu za Simba, Yanga, Singida United, Jang’ombe Boys, AFC Leopards, Tusker FC, Gor Mahia na Nakuru All Stars ndio zitashiriki michuano hiyo na moja kati ya timu hizo itacheza na Everton.


ame ya Everton itakuwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam na ujio wao Tanzania ni sehemu yao ya makubaliano yao ya udhamini na SportPesa, mtandao wa liverpoolecho.co.uk ni moja kati ya mitandao mikubwa katika jiji la Liverpool ambapo inatokea timu ya Everton.

RC Shinyanga azuiwa kuingia mgodini



Msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Tellack, umezuiwa kuingia katika mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu alikokwenda kukagua iwapo uzalishaji unaendelea bila kuwepo kwa Maofisa wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini, TMAA.

Maofisa wa TMAA waliondoka mara baada ya ripoti ya uchunguzi wa mchanga wa dhahabu kukabidhiwa kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli hapo jana ikulu jijini Dar es sallaam.

Bi. Zainabu amesema ameagiza Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi katika eneo lote la mgodi huo kuhakikisha hakuna mtu anayetoka wala kuingia

Mapema leo Mkuu huyo wa Mkoa alitembelea mgodi mwingine wa Buzwagi ambao pia unamilikiwa na kampuni ya Acacia kama ulivyo ule wa Bulyanhulu.

Katika mgodi wa Buzwagi, Bi. Zainab na msafara wake waliruhusiwa kuingia na kushuhudia shughuli za uchimbaji zikiwa zimesitishwa kwa kukosekana maofisa wa TMAA walioondoka mara baada ya Rais Magufuli kutangaza kuvunja bodi na kutengua uteuzi wa watendaji wakuu wa wakala hiyo.

The President of United Republic of Tanzania Remove Minister Following Investigation on Mineral Sand Exports



Government of Tanzania has released yesterday the report of the Presidential Committee’s investigation into the contents of gold, copper and other minerals in the mineral sand in containers for export.

 The report, in Swawili, identifies major discrepancies in the average concentration of these minerals, per ton of mineral sand, resulting in losses of revenue from royalties.
 Gold The Committee has identified large quantities of gold between 671 g / t to 2,375 g / t, equivalent to an average of 1400 g / t. This average is equivalent to 28 kg of gold in a container with 20 tons of gold ore.

Thus, the 277 containers of mineral sand blocked at the Port and Dry Port of Dar es Salaam and will have approximately 7.8 tons of gold worth TZS 676 billion (USD 307 292 720), the report explains.
The committee reminds that the Tanzania Minerals Audit Agency (TMAA), the government’s body responsible for monitoring and auditing of mining operations, recorded an average gold concentration of 200 g / t, equivalent to 4 kg of gold per container.
 Copper The average amount of copper identified in the 277 containers is 1440.4 tons which is worth TZS billion 17.9 (USD 8,138,260).
However, shipping documents that the Committee received from port revealed that the average rate of copper is equal to 4 tons of copper in each container, equal to 1,108 tons of copper for 277 containers with a value of TZS 13.6 billion (USD 6,204,800).

Other Minerals The Committee also analyzed and identified discrepancies in the concentration and value of other minerals, including silver, sulfur, iron, iridium, rhodium, ytterbium, beryllium, tantalum, and lithium.

 In its recommendations, the Committee advises the government to maintain the suspension shipment of mineral sand abroad unless royalties are paid based on the real value of concentrate as outlined in the investigation.

Also, it advises TMAA to seal the containers immediately after sampling to avoid frauds that can happen afterward. The Committee finally advises the government to ensure that the construction of smelters in the country takes place as soon as possible. 

Following the presentation of the results of the investigation, on the same day, President Magufuli revoked the appointment of the Minister of Energy and Mines Prof. Sospeter Muhongo, with immediate effect. The president also dissolved TMAA board of directors and suspended TMAA Chief Executive Officer. 

Tanzania Mineral Concentrates Exports Ban Tanzania issued a ban on the export of mineral concentrates and ores for metallic minerals such as gold, copper, nickel and silver, with effect from 2nd March 2017, and established two special committees to examine the extent, types and values of minerals contained in mineral sand in containers for export in various locations in the country. 

The ban heavily affected Tanzanian gold producer Acacia Mining (LSE:ACA) who reported a reduction in sales of almost 35,000 ounces lower than production in its results for Q1 2017, because of the ban, the company explains.

 Following the release of the investigation yesterday, Acacia re-iterated that it fully declares everything of commercial value that it produces and pays all appropriate royalties and taxes on all of the payable minerals that it produces. The company also indicates that it will provide a further update to the market as soon as practical.


Sunday, May 14, 2017

Hiki Ndicho Alichosema MO kwa simba




Baada ya  simba na SportPesa Tanzania rasmi  kutangza udhamini wake wa miaka mitano kwa klabu ya Simba ya Dar es Salaam, wenye thamani ya Sh. Bilioni 4.96.

MO kawaandikia Simba ‘demand note’ kwa kua wamekiuka makubaliano yao kwamba, atoe pesa kama makubaliaono ya kuingia kwenye mfumo wa hisa na ikitokea kampuni inataka kuidhamini Simba inabidi wakae meza moja viongozi na MO ili hiyo kampuni itambue mwelekeo wa Simba, lakini viongozi wa klabu hiyo wakasaini kimyakimya.

Simba ilishaanza mchakato wa marekebisho ya katiba yao ili kuruhusu kipengele cha uwekezaji kwa mfumo wa hisa kama lilivyokua ombi la MO kuwekeza katika klabu hiyo kwa asilimia 51 za hisa huku wanachama wakibaki na hasilimia 49.
Adi kufikia leo akuna majibu yoyote yaliotoka simba na hiki ndicho alichokiandika Mo kwenye hukurasa wake wa instagram



"Inasikitisha kuwa uongozi wa Klabu ya Simba umesaini mkataba wa udhamini wa muda mrefu bila kunishirikisha. Kwa muda mrefu nimeweka nguvu zangu kwenye klabu."


Saturday, May 13, 2017

Taarifa Kuhusu Hali ya Saimoni Msuva




Nyota  wa timu ya yanga Msuva alipata jeraa  wakati wa mpambano wao zidi ya mbeya city uluiofanyika  uwanja wa taifa jijini Dar es salaam huko yanga kuibuka  na ushindi mnono wa ngili mbili  kwa moja ,Yanga ndio walioanza kuongoza kwa ngoli moja lilo fungwa na   Msuva  kupelekea kuchanika juu ya jicho lake la kushoto ambapo ameshonwa nyuzi nne baada ya kugongana na mchezaji wa Mbeya city wakati akifunga goli lake la 14 kwenye ligi kuu Tanzania bara msimu huu.

 YANGA SC imerudi kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kutokana na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City ya Mbeya jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo unawafanya mabingwa hao watetezi watimize pointi 65 baada ya kucheza mechi 28 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu. Simba inaangukia nafasi ya pili kwa pointi zake 65 za mechi 29, ikizidiwa wastani wa mabao.  

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Andrew Shamba wa Pwani, aliyesaidiwa na Joseph Pombe wa Shinyanga na Haji Mwalukuta wa Tanga, dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika Yanga ikiwa inaongoza 1-0.

Hata hivyo, Yanga wakafanikiwa kupata bao la pili lililofungwa na mshambuliaji Mzambia, Obrey Chirwa dakika ya 64 akimalizia mpira wa adhabu wa Juma Abdul.

Mbeya City ilijitahidi kujaribu kusawazisha bao hilo, lakini tayari wapinzani wao, Yanga walikuwa wamekwishaanza kucheza kwa kujihami zaidi na kushambulia kwa kushitukiza.

Mrisho Ngassa aliingia kipindi cha pili upande wa Mbeya City, lakini hakuwa na madhara kwa timu ya timu yake ya zamani zaidi tu ya kusisimua mashabiki kwa uchezaji wake mzuri. 

Kikosi cha Yanga; Benno Kakolanya, Hassan Kessy/Emmanuel Martin dk, Mwinyi 
 Hajji Mngwali, Vincent Bossou, Nadir Haroub ‘Cannavaro’/Kevin Yondan dk67, Thabani Kamusoko, Simon Msuva/Juma Abdul dk12, Haruna Niyonzima, Amisi Tambwe, Obrey Chirwa na Geoffrey Mwashiuya.

Mbeya City; Owen Chaima, Haruna Shamte, Hassan Mwasapili, Tumba Lui, Sankani Mkandawile, Kenny Ally, Ditram Nchimbi, Majaliwa Shaaban, Zahor Pazi/Bryson Raphael dk46, Raphael Daudi na Rajab Isihaka/Mrisho Ngassa dk58.

Waspania wa Mkubali Farid Mussa Malik na wakisema hiki


MAKOCHA wa timu ya vijana ya Deportivo Tenerife wamemuambia winga wa kimataifa wa Tanzania, Farid Mussa hana muda mrefu kabla ya kuanza kucheza Ligi kubwa Ulaya.


Hiyo inafuatia makocha hao kuvutiwa na kiwango cha mchezaji huyo katika mechi zake za timu ya vijana DC Tenerife ya Hispania.

Akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online kwa simu leo kutoka Hispania, Farid amesema kwamba juzi baada ya kufunga mabao mawili na kutoa pasi moja ya bao katika ushindi wa 5-1 Uwanja wa Heliodoro Rodriguez walimpongeza sana na kumuambia atafika mbali.

“Juzi nilifunga mabao mawili na kutoa pasi moja ya bao, baada ya mechi wakanifuata kwa furaha na kuniambia mimi ni mchezaji mkubwa wa baadaye, sina muda mrefu nitacheza ligi kubwa. Kwa kweli imenifariji sana na kunitia moto wa kujituma zaidi,”amesema Farid.

Kwa wiki hii peke yake, Farid amefikisha mabao matatu baada ya Jumatatu kufunga bao moja na kutoa pasi moja ya bao katika ushindi wa 3-0.

Farid alijiunga na klabu hiyo ya Santa Cruz de Tenerife, Tenerife, visiwa vya Canary Desemba mwaka jana kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu kutoka Azam FC ya Dar es Salaam.
Azam FC ilimtoa kwa mkopo Farid kwenda CD Tenerife kwa makubaliano maalum baada ya winga huyo kufuzu majaribio katika klabu hiyo Aprili mwaka jana alipokwenda na Mkurugenzi wa klabu yake, Yussuf Bakhresa.

Farid alitua Hispania kwa mara ya kwanza Aprili 21, mwaka jana baada ya kuichezea Azam FC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance mjini Tunis, Tunisia ikifungwa 3-0 na kutolewa kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya awali kushinda 2-1 Dar es Salaam.


Na ilimchukua wiki moja tu Farid kuwakuna kwa kipaji chake makocha wa Tenerife na kutaka kumnunua, lakini Azam ikakataa na kuamua kumtoa kwa mkopo Desemba, 2016.


Na baada ya kutua Tenerife akapangiwa kuanza kuchezea kikosi cha U-20 ili kupata uzoefu kabla ya kupandishwa kikosi cha kwanza kinachocheza Segunda, Ligi ya pili kwa ukubwa Hispania.

President of united Republic of Tanzania Reiterate Support to Tanzania Private Sector But Tax Compliance Remain Key



The President of Tanzania, Hon. Dr. John Magufuli hosted on 6th May 2017 the National Business Council (TNBC) – a forum for public and private sector dialogue – at the White House in Dar es Salaam.


Launched in 2001, the dialogue aims to reach consensus and mutual understanding on strategic issues relating to the efficient management of resources in the promotion of social economic development in Tanzania.

During the forum President Magufuli reiterated its Government’s commitment to cooperate with the private sector in planning and implementation of plans, policies and various laws on investment and business, and to remove barriers and bureaucracy that hinder trade and investment.

Following complaints about delays in cargo handling at the Dar Es Salaam port President Magufuli has ordered, during the forum, that from the 8th of May 2017 all the government institutions that offer services at the port of Dar es Salaam to operate 24 hours a day, 7 days a week. The institutions concerned include the Tanzania Revenue Authority (TRA), the Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA) and the Tanzania Bureau of Standards (TBS).

 However, President Magufuli also urged businessmen and investors to comply with their tax duties, avoid engaging in corruption and raising the price of the services provided to the government.


 Since coming to power in November 2015, President Magufuli has been praised by the business community for its crackdown on corruption.

 He has also made tax compliance and collection a key point of his administration. However, he is often criticized for the hefty austerity measures he has introduced that have heavily reduced government spending on the private sector, and for the lack of engagement with the business community.


Wednesday, May 10, 2017

HIMID MAO APEWA DAKIKA 90 DENMARK TIMU YAKE YAPIGWA 2-0


 Himid Mao Mkami leo amejumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji wa akiba na timu ya Randers FC ya Denmark na kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Horsens.

Kiungo huyo wa Azam FC ya Dar es Salaam ambaye yupo Denmark kwa majaribio ya kujiunga na timu hiyo ya Ligi Kuu, amecheza kwa dakika zote 90 na kwa bahati mbaya wachezaji wa akiba wa Randers FC wakafungwa 2-0.


" Himid amesema kwamba ulikuwa mchezo mgumu, lakini upande wake anamshukuru Mungu amecheza vizuri."

“Unajua kufungwa haimaanishi mmecheza vibaya, wakati mwingine mnaweza kucheza vizuri kuliko waliowafunga, sema basi tu mambo ya mpira,”amesema Himid, mtoto wa kiungo wa zamani wa Pamba, Mao Mkami ‘Ball Dancer’.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Tanzania amesema baada ya kufanya mazoezi na timu hiyo kwa takriban siku tatu na leo kucheza mechi ya kwanza – kesho anatarajiwa kupewa ratiba mpya.


Himid amesema anaamini baada ya kucheza Tanzania kwa muda mrefu, sasa ni wakati mwafaka kwake kutoka nje.
“Ni kweli nina nia sana ya kutoka nje kwa sasa, naamini ni wakati mwafaka kwangu kupata changamoto mpya katika maisha yangu ya soka,”amesema Nahodha huyo Msaidizi wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.   

Big Opportunity International Mobile Money Transfer Now Available in Tanzania




International mobile payment network TerraPay has obtained regulatory approval from the Bank of Tanzania (BOT) to launch international money transfer services to mobile wallets in Tanzania.

This is the first license of its kind in Tanzania, allowing TerraPay’s partners across the world to send money directly to mobile wallets in Tanzania.

 Through a partnership with Tanzanian mobile money aggregator Selcom, TerraPay can send money to all the prominent mobile wallets in Tanzania.

 Tanzanian diaspora in UK, France, Italy, Canada, US, South Africa and other countries can now send remittances directly to Vodacom M-Pesa, Tigo Pesa, Airtel Money and Zantel Ezy Pesa mobile money accounts, TerraPay explains. Furthermore, the company has also been licensed by the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) for mobile-based domestic payments. According to World Bank (WB), Tanzania received a total of USD 390 million in 2015 from over 4 million expatriates living abroad.

 Mr. Ambar Sur, Founder & CEO of TerraPay commented “Tanzania is one of the fastest growing country in mobile wallet space with a total of 18 million active mobile money subscribers.

The Bank of Tanzania’s recent move to provide TerraPay with a license to send international remittances to mobile wallets in the region will provide a boost to remittances in Tanzania. We are positive that other partners will join the TerraPay hub which will help to grow and sustain remittances to mobile wallet in the region.


” TerraPay is registered and regulated in several jurisdictions. In the UK, it is regulated by the Financial Conduct Authority (FCA).


Wednesday, May 3, 2017

Viongozi kutoka Ukanda wa CECAFA wakubaliana kuimarisha soka



Marais kutoka mataifa yanayounda Baraza la soka Afrika Mashariki CECAFA, walikutana jijini Kampala nchini Uganda siku ya Jumatano kuzungumzia namna ya kuboresha mchezo wa soka katika ukanda huo.
Mkutano huo ulihudhuriwa na marais saba wakiongozwa na mwenyeji wao Moses Magogo, Vincent Nzamwita kutoka Rwanda, Jamal Malinzi (Tanzania), Juneidi Tilmo (Ethiopia), Nicolas Mwendwa (Kenya) na Ndikuniyo Reverien (Burundi).
Ravia Faina rais wa Shirikisho la soka kutoka kisiwa cha Zanzibar kilichopewa uanachama wa CAF hivi karibuni, pia alikuwepo.
Mambo saba yaliyoafikiwa katika mkutano huo ni pamoja na:-
1 – Kuibadilisha Katiba ya CECAFA.
2 – Kuandaa mkutano mkuu wa CECAFA haraka iwezekanavyo.
3 – Kuhakikisha kuwa CECAFA inapata Makao makuu ya kudumu.
4 – Kuimarisha michuano ya vijana wasiozidi miaka 15, 17 na 20 kwa wavulana na wasichana pamoja na kuboresha soka la ufukweni.
5 – Kuimarisha hali ya waamuzi uwanjani, makocha, uongozi lakini pia hali ya matibabu kwa wachezaji.
6 – Kuimarisha mawasiliano na kuitangaza CECAFA.
7 – CECAFA kuomba nafasi ya kuandaa fainali ya mataifa bingwa barani Afrika katika siku zijazo.
8 –CECAFA kuwakilishwa ipasavyo katika Kamati kuu ya CAF.
9 –Kuja na mbinu za kuandika mapendekezo kwa Shirikisho la soka duniani FIFA ili kusaidia kuinua soka la vijana, wanawake na lile la ufukweni.

Mkwasa asema aina mpango wa kuwatema wachezaji Yanga


Bonifasi Mkwasa Katibu Mkuu wa Yanga

Katibu Mkuu wa Yanga SC,  Charles Boniface Mkwasa amekanusha taarifa zinazoendelea kusambazwa katika mitandao ya kijamii kwamba wana nia ya kuwaacha baadhi ya wachezaji wake na kusema hizo taarifa na uzushi mkubwa ndani ya klabu yao.


Mkwasa amebainisha hayo kupitia taarifa yake aliyoitoa asubuhi ya leo baada ya kuenea kwa taarifa kutoka baadhi ya vituo vya Radio na 'social network' zikidai klabu hiyo inataka kuwabwaga baadhi ya wachezaji wake kutokana na kufanya vibaya katika Ligi.
"Taarifa hizo ni za uongo na uzushi mkubwa, uongozi upo bega kwa bega na wachezaji wote 27 na benchi la ufundi. Hatujakaa kulijadili hilo wala kulifikiria bali tupo makini kutetea ubingwa wetu wa ligi kuu". Alisema Mkwasa
Aidha, Mkwasa alisisitiza kwamba Kocha Mkuu, George Lwandamina ndiyo mwenye maamuzi ya mwisho juu ya huduma ya wachezaji ndani ya klabu hiyo na wala siyo kiongozi mwingine yoyote
"Kocha Mkuu George Lwandamina hajatoa taarifa yoyote ya kumwacha mchezaji gani au yupi wa kumuongezea mkataba,  zaidi ya kila siku kuukazia uongozi kuboresha masilahi ya wachezaji kwa sababu kama kocha mkuu anajivunia na kujali kazi ya vijana wake". 

Himid aka Niinja kwenda Ulaya kutafuta maisha ya soka la kulipwa


himid mao akiwa Denmark ndani ya uwanja wa timu ya Randers FC

Kiungo wa Azam FC  na timu ya taifa ya Tanzania Himid Mao ameondoka nchini jioni ya leo Mei 1, 2017 kuelekea Denmark kwa ajili ya majaribio ya kutafuta kucheza soka la kulipwa barani Ulaya.
Himid anakwenda kwenye klabu ya Randers FC inayoshiriki ligi kuu nchini humo ligi inayojulikana kwa jina la Superliga.

Kiungo huyo ameonesha kiwango cha juu katika msimu huu kuanzia kwenye mechi za ligi kuu Tanzania bara, kombe la Azam Sports Federation Cup, michuano ya kimataifa pamoja na mechi za timu ya taifa.shaffihdauda.co.tz ilizungumza na Himid Mao muda mfupi kabla hajaondoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Nyerere.
“Naenda kwenye klabu ya Randers FC ya nchini Denmark kwa ajili ya majaribio kwa muda wa siku 15, kama mchezaji najiamini naweza kufanya lolote sehemu yoyote, mambo mengine ya mbeleanajua Mungu,” amesema Himid muda mfupi kabla ya kuondoka ardhi ya Bongo.

“Mimi wajibu wangu ni kujitolea kadiri niwezavyo na kuwashawishi hao kwa uwezo wangu wote patakapobakia ni kazi ya Mungu.”
“Kila kitu kipo kama kilivyopangwa, klabu yangu inajua, wakala anajua kwa hiyo kila kitu kipo wazi utakapofika wakati wa klabu kutangaza chochote watafanya hivyo.”

“Kwa sasa naangalia hiki kilichopo mbele halafu baadae tutajua nini kitakachofuata.”
Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com