Featured
Showing posts with label sport. Show all posts
Showing posts with label sport. Show all posts

Friday, August 12, 2016

MO BAJAIA WATUA, WAETHIOPIA KUAMUA, VIINGILIO VYATAJWA




Jumla ya kikosi cha watu 35 ambao ni wachezaji na viongozi wa MO Bajaia kutoka Algeria, wametua Dar es Salaam, usiku wa kuamkia jana Agosti 9, 2016 na imefikia Hoteli ya Ledger Plaza, iliyoko Kunduchi Beach nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Timu hiyo imekuja kucheza na Young Africans ya Dar es Salaam, katika mchezo wa nne wa hatua ya Nane Bora kuwania Kombe la Shirikisho Barani Afrika utakaofanyika Jumamosi Agosti 13, 2016 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Licha ya kwamba Young Africans kuwa na pointi moja, bado ina nafasi ya kushika nafasi za juu katika kundi la A ambalo msimamo wake unaongozwa na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), huku Mo Bajaia ya Algeria na Medeama ya Ghana, zina pointi tano kila moja. Wakati Young Africans wanacheza na Mo Bajaia iliyoshinda mchezo wa kwanza huko Algeria, Medeama itakipiga na TP Mazembe.

Mchezo wa Young Africans dhidi ya Mo Bajaia utachezeshwa na waamuzi kutoka Ethiopia ambako katikati atakuwa Bamlak Tessema Weyesa akisaidiwa na Kindie Mussie mstari upande wa kusini na Temesgin Samuel Atango katika mstari wa Kaskazini upande wa wakati Mwamuzi wa Akiba atakuwa Haileyesus Bezezew Belete.

Kamishna wa mchezo atakuwa Gaspard Kayijuka kutoka Rwanda wakati Desire Gahuka wa Burundi atasimamia ufanisi wa waamuzi wa mchezo na Mratibu Mkuu wa mchezo atakuwa Isam Shaaban kutoka Sudan. Mratibu huyo anatarajiwa kuwasili leo Agosti 10, 2016 wakati waamuzi watatua kesho Agosti 11, 2016 na msimamizi wa waamuzi atatua Ijumaa Agosti 12, 2016.


Kiingilio katika mchezo huo kitakuwa ni Sh 3,000 kwa mzungunguko kwa maana ya viti vya kijani, bluu na chungwa wakati Viti Maalumu vyenye hadhi ya daraja B na C kiingilio kitakuwa Sh 10,000 wakati A kiingilio kitakuwa ni Sh 15,000 kwa mujibu wa Waratibu wa Young Africans.

HUMUD AFUATA NYAYO ZA NGASSA, UHURU, ASAINI AFRIKA KUSINI




KIUNGO  wa zamani wa Ashanti United, Mtibwa Sugar, Simba SC na Azam FC amesaini mkataba wa mwaka mmoja katika timu ya Real Kings FC. Humud ambaye alikuwa nahodha wa Coastal Union ya Tanga ambayo iliteremka daraja msimu uliopita amejiunga na timu hiyo ya daraja la kwanza Afrika Kusini kama mchezaji huru.
“Ni kweli nimesaini Kings,” anasema mchezaji huyo wa nafasi ya kiungo wa kati ambaye alitabiriwa mambo makubwa wakati akichipukia Ashanti mwaka 2007.
“Nina mategemeo makubwa ya kufanya vizuri na kuisaidia timu yangu kupanda ligi kuu msimu ujao.” anasema Humud ambaye alipiga mpira wa kiwango cha juu mno wakati Taifa Stars ilipocheza na timu za Taifa za Ivory Coast na Brazil mwaka 2010.

Sasa anakuwa mchezaji wa tatu Mtanzania anayecheza Afrika Kusini akifuata nyazo za Mrisho Ngassa na Uhuru Suleimani Mwambungu.

Tuesday, August 9, 2016

DIRISHA LA USAJILI VPL...




Dirisha la usajili kwa timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Ligi Daraja la Kwanza la StarTimes na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2016/2017 lilifungwa saa 6.00 usiku wa Jumamosi Agosti 6, 2016.
Hadi dirisha linafungwa, timu kadhaa hazikuwasilisha kabisa usajili wake licha ya kukumbushwa kwa njia mbalimbali na uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).


Usajili wa msimu huu ni kama msimu uliopita kwamba unafanyika kwa njia au mfumo wa mtandao unaoitwa Transfer Matching System (TMS) ambao (server) yake au chombo chake cha kutunza kumbukumbu kipo Makao Makuu ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) - Uswisi.

Kwa kawaida mfumo huu upo chini ya FIFA na TFF hutoa taarifa kwa FIFA tarehe ya kufungua dirisha la usajili na kufunga.

Mfumo huu uhusisha pande tatu ambazo ni klabu, shirikisho (TFF) na FIFA. Kimsingi kazi ya usajili hufanywa na klabu ambako inajaza fomu kwa njia ya mtandao na hupakia viambatanisho kama vile mikataba ya wachezaji na picha za wachezaji.

Zoezi hili hufanywa na Meneja Usajili wa klabu husika wakati shirikisho hufanya kazi ya kuhakiki na kuidhinisha tu na FIFA huratibu na kuusimamia mfumo mzima. 

Kabla ya kutangaza kufunguliwa kwa dirisha la usajili hapo Juni 15, 2016 Shirikisho liliandaa kozi ya mafunzo ya usajili kwa klabu zote 64 zikiwa ni 16 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara; 24 zitakazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza la StarTimes na timu 24 zitakazoshiriki Ligi Daraja la Pili msimu wa 2016/2017.

Baadhi ya timu hazikutuma wawakilishi, lakini ziko zilizofanya jitihada za kuomba usaidizi kwa kufika ofisini TFF kuomba usaidizi wa kufanya usajili na zilifanikiwa. Kwa Young Africans, licha ya kuwa hapa Dar es Salaam, haikuomba usaidizi wowote na hata walipokumbushwa kuhusu suala la usajili, hawakujibu kitu.

Young Africans ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mara mbili mfululizo msimu wa 2014/2015 na 2015/2016, ni moja ya vilabu ambavyo havikutuma mwakilishi kwenye kozi iliyofanyika Uwanja wa Taifa kwa siku tatu mfululizo ikigusa wawakilishi wa madaraja ya Ligi Kuu, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili.

Meneja wa TMS wa Young Africans ni Katibu Mkuu hakuwahi kupata mafunzo ya TMS.

Hivyo sasa klabu zote ambazo hakuzituma usajili wake, hazina budi kuandaa utetezi utakaokwenda TFF ambao utatumwa FIFA yenye mamlaka ya kufungua dirisha, na utetezi huo ukikataliwa timu husika inabidi ishuke daraja ambalo halimo kwenye usajili wa mfumo wa TMS.


TFF kwa sasa inasuburi barua ya utetezi wa klabu ambazo hazikukamilisha zoezi la usajili ili iutume FIFA. Sambamba na hilo TFF inatathimini mwenendo mzima kisha itatoa taarifa kwa FIFA ili kuangalia namna gani ya kushughulikia maeneo yaliyokuwa na upungufu kwa sasa na baadaye. 

Sunday, August 7, 2016

Serengeti Yatoshana Nguvu na Afrika Kusini kwao




Afrika Kusini iliyopania kupata ushindi kwao, kwenye Dimba la Dobsonville, Soweto jijini Johannesburg, imeshindwa kutamba mbele ya vijana Watanzani Serengeti Boys baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa kwanza wa kuwania nafasi ya kucheza Kombe la Mataifa Afrika.
Wenyeji walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Luke Gareth kwa penalti baada ya mchezaji mmoja wa Serengeti Boys kumfanyia madhambi ndani ya 18 Gareth katika dakika ya 65. Lakini dakika ya 70, Ally Msengi aliisawazishia Serengeti Boys bao pia kwa penalti iliyotokana na Beki, Sechaba Makoena kushika mpira ndani ya eneo la hatari. Mwamuzi wa mchezo alikuwa William Koto kutoka Lesotho.
Kwa matokeo ayo nimwanzo mzuri kwa upande wa timu ya serengeti boys ambayo italazimika kusubi duru ya pili itakayo chezwa hapa Tanzania.
Mchezo wa marudiano utachezwa Agosti 21, kwenye uwanja wa Azam Compolex, Chamazi, Dar es Salaam. Endapo Serengeti Boys itafanikiwa kuitupa nje ya mashindano timu ya vijana ya Afrika Kusini, itatinga hatua ya mwisho ya mchujo kabla ya kufuzu kwa ajili ya fainali hizo.

Saturday, August 6, 2016

Nafasi Ya Tanzania Ndani ya Olimpiki





Leo Agosti 5, 2016, michezo ya 31 ya Olimpiki itafunguliwa rasmi jijini Rio nchini Brazil. Tanzania itakuwepo!
Katika michezo ya mwaka huu, Tanzania itawakilishwa na wanamichezo saba; wanariadha wanne, waogeleaji wawili na mwanajudo mmoja. Timu ya Tanzania inakwenda Rio kinyonge tena kwa mafungu mafungu huku nyuso za mashujaa wetu zikihadithia simulizi tofauti na ndimi zao. Ndimi zimeahidi medali lakini nyuso zimekataa. Tanzania inasikitisha!
Hii ni tofauti na ilivyokuwa miaka 40 iliyopita, 1976, siku moja kabla ya ufunguzi wa michezo ya Olimpiki. Tanzania ilikuwa Tanzania kweli kweli. Tanzania ilikuwa moto!
Siku hiyo ilikuwa Julai 16, 1976, siku moja kabla ya kufunguliwa rasmi kwa michezo ya 21 ya Olimpiki huko Montreal Canada, (kama ilivyokuwa jana, siku moja kabla ya ufunguzi wa Olimpiki ya Rio) dunia ilipata mtikisiko kwa kauli moja tu kutoka Tanzania, “HATUTASHIRIKI OLIMPIKI MWAKA HUU”. Tanzania ilikuwa thabiti.
Kauli hiyo iliyotolewa na Ikulu ya Magogoni, ilipeleka mwangwi dunia nzima na kuzua mtikisiko mkubwa uliopelekea mataifa 28 ya Afrika na mengine matano kutoka nje ya Afrika, kuitikia wito wa Tanzania wa kususia michuano hiyo. Kati ya mataifa hayo, 20 yalikuwa tayari yameshawasili Montreal lakini yakaitikia wito wa Tanzania na kurudi majumbani kwao. Tanzania ilisikilizwa. Tanzania iliheshimika!
Tido Mhando, mtangazaji wa kipindi cha michezo RTD wakati huo, ambaye alikuwa asafiri na timu ya Tanzania, anakumbuka vizuri tukio hilo.
“Tulikuwa tumejiandaa vizuri. Tanzania ilikuwa na timu ya wachezaji zaidi ya 40 akiwemo Filbert Bayi ambaye alikuwa nyota mkubwa kabisa duniani. Wakati huo, ukiwataja wanamichezo maarufu duniani, utamzungumzia Muhammad Ali kwenye masumbwi, Yohan Cruyff kwenye mpira na Filbert Bayi kwenye riadha. Na kwa kuwa hao wengine hawakushiriki Olimpiki, Filbert Bayi ndiyo alikuwa nyota mkubwa zaidi kwenye Olimpiki hizo”. Tanzania iliheshimika. Tanzania iliogopewa!
Kwa maelezo ya Tido, Bayi alitoka kushinda medali ya dhahabu ya michezo ya Jumuiya ya Madola huko Christchurch New Zealand 1974 ambako aliweka rekodi ya dunia ya mbio za mita 1500 akitumia muda wa dakika 3 na sekunde 32.16, rekodi ambayo imedumu mpaka sasa. Kikubwa hapa hakikuwa tu rekodi bali mtindo alioutumia kuiweka…Bayi alikimbia kwa kasi ileile tangu anaanza mpaka anamaliza akimuacha mpinzani wake wa karibu, John Walker, aliyekuwa uwanja wa nyumbani. Tanzania ilitikisa!
“Nikiwa kama mtangazaji wa michezo, nilipewa taarifa kwamba kuna kikao kikubwa cha serikali kikiongozwa na Rais, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kujadili hatima ya Tanzania kwenye olimpiki hizo. Hayupo aliyejua kwamba kikao hicho kitatoka na kauli gani hivyo mimi binafsi kama mwanahabari na wanamichezo washiriki tuliambiwa tuwe tayari tayari kwa lolote. Baadaye zikaja taarifa kwamba serikali imeamua kutoshiriki. Taarifa hizo nikazi-break mimi kupitia kipindi changu cha michezo na hapo hapo zikasambaa duniani. BBC na mashirika mengine makubwa duniani yakaninukuu….kilichofuata baada ya hapo ni hasara kubwa kwa jiji mwenyeji la Montreal. Wanamichezo zaidi ya 300 walijiondoa na kusababisha michezo mingi kufutwa”. Anakumbuka Tido Mhando ambaye sasa ni afisa mtendaji mkuu wa Azam Media.
Kisa cha Tanzania kususia michezo hiyo ni kupinga kitendo cha kamati ya kimataifa ya Olimpiki, IOC, kuiruhusu New Zealand kushiriki Olimpiki hizo ilhali ilikiuka maagizo yake ya kuitenga Afrika Kusini kutokana na sera zake za ubaguzi wa rangi.
Afrika Kusini ilitengwa na IOC tangu 1964, lakini timu ya taifa ya ragga ya New Zealand (All Blacks) ilifanya ziara ya kirafiki nchini humo. Kitendo hicho kilitafsiriwa kama kupuuza maagizo ya dunia ya kuitenga Afrika Kusini.
Tanzania kama kinara wa kupinga ubaguzi, ilikuwa ikisubiriwa itakuja na tamko gani…hatimaye tamko likatoka na kuitikiwa barabara.
Tanzania iliyokuwa na nyota mkubwa kabisa, Filbert Bayi, ilikuwa ikitazamwa kama moja ya mataifa yatakayong’arisha Olimpiki hiyo.
Jaribu kuifikirikia Tanzania ya sasa yenye timu ya wanamichezo saba tu. Wanamichezo wenye majina madogo, siyo tu kimataifa bali hata kitaifa. Siyo ajabu katika watu kumi, ni mtu mmoja pekee akawa anawajua wawakilishi wetu.
Tanzania hii inaweza kweli kutoa kauli itakayoitikiwa na umma wa kimataifa?

Tanzania hii inaweza kweli kichukuliwa kama moja ya mataifa yatakayong’arisha michezo hiyo?

ARSENAL YAPATA MAJERUI KUELEKEA EPL DHIDI YA LIVERPOOL




Mesut Ozil, Laurent Koscielny na Olivier Giroud wote watakosa mchezo wa ufunguzu wa Lifi Kuu ya England dhidi ya Liverpool, kocha Arsene Wenger amethibitisha.
Watatu hao hawakushiriki mazoezi na wenzao baada ya Michuano ya Euro mwaka huu kumalizika na hivyo Wenger ameamua kutowajumuisha kwenye kikosi chake kitakachowaa vijana hao wa Jurgen Klopp kwenye dimba la Emitares.
Akiongea baada ya ushindi wa magoli 8-0 katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Viking jana, Wenger alisema: “Itakuwa mapema mno kuwachezesha katika mchezo dhidi ya Lverpool.”
Kukosekana kwa Giroud kunamfanya Wenger kubakiwa na mastrika wawili ambao ni Theo Walcott na Chupa Akpom.
Walcott alianza kuziona nyavu kwenye mchezo wa jana dhidi ya Viking, huku Akpom naye akizidi kuonesha kile kinachotakiwa na straika kuelekea msimu mpya wa ligi baada ya kufunga goli lake la tatu katika michezo ya kirafiki.

Joel Campbell na Alex Iwobi walifunga magoli mawili kila mmoja. huku Santi Cazorla na goli lingine la kujifunga likiwazamisha Viking.

Friday, August 5, 2016

Serengeti Boys Yawasili Salama nchini Africa Ya Kusini.......





Serengeti Boys, yawasili salama Johannesburg kwa ajili ya mchezo dhidi ya wenyeji afrika Kusini utakao pigwa jumamosi ya kesho , Timu sasa itafikia Garden Court badala ya Protea Rooddepoort hapa Johannesburg.
serngeti boys wakifanya mazoezi mepesi wakiwa afrika Kusini
Ni hii ni timu ya soka ya Taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17, kesho Jumamosi inajitupa katika Dimba la Dobsonville, liliko Soweto hapa jijini Johannesburg kuifumua Afrika Kusini katika mchezo wa kuwania tiketi ya kucheza Kombe la Mataifa ya Afrika
.
Kikosi kiko vema, kwa kuona tu pia kwa maelezo ya makocha, Bakari Shime na Juma Kaseja pamoja na Daktari Shecky Mngazija. Dua zenu Watanzania.

Thursday, August 4, 2016

Barcelona 4-2 Leicester City: Ahmed Musa afunga mabao mawili





Mchezaji ghali zaidi kununuliwa na Leicester City Ahmed Musa, aliyenunuliwa pauni milioni 16 na kuvunja rekodi ya klabu hiyo, amewafungia mabao yote mawili katika mechi ambayo wamefungwa 4-2 na Barcelona katika michuano ya Kombe la Kimataifa la Klabu.
Munir alifungua ukurasa wa mabao kupitia pasi iliyotoka kwa Lionel Messi kabla ya nyota huyo wa Argentina muda mfupi baadaye kumuandalia pasi safi Luis Suarez aliyeongoeza la pili katika mchezo huo uliochezewa uwanja wa Friends Arena mjini Stockholm, Sweden.
Munir aliongeza la tatu, kabla ya Musa kukomboa bao moja.
Musa alifanikiwa kukomboa la pili lakini nguvu mpya wa Barca Rafa Mujica, mwenye umri wa miaka 17 pekee, akaifungua Barcelona la nne dakika za mwisho mwisho.
"Msimu uliopita Leicester walishangaza sana katika soka ya Ulaya, na hii ndiyo sababu inayomfanya kila mtu kuupenda mchezo huu," meneja wa Barcelona Luis Enrique alisema baadaye.

Wednesday, August 3, 2016

AUDIO: Ukweli kuhusu stori za Kavumbagu kuripotiwa kufungiwa na FIFA




Najua utakuwa ilisikia stori za mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi aliyekuwa anaichezea klabu ya Azam FC Didier Kavumbagu kuripotiwa kufungiwa na shirikisho la soka ulimwenguni FIFA  kutokana na kudaiwa kusaini timu mbili tofauti ndani ya Ligi ya Vietnam, stori zilienea sana lakini Kavumbagu kaweka ukweli wote Sports Extra ya Clouds FM.
“Ukweli sijafungiwa ila kuna matatizo ya mikataba yalinikuta Vietnam timu iliyokuwa imeeniita nilikuta imemsajili mbrazil kutokana na mimi kuchelewa kufika, lakini nilitafutiwa timu nyingine nikafuzu majaribio na kusaini mkataba baadae wakagombana na meneja wangu nikaenda timu nyingie FIFA wakasema mchezaji mmoja hawezi saini mkataba timu mbili”

Azam FC yashusha mshambuliaji kutoka Ivory Coast




klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC , leo imemshusha  mshambuliaji kutoka Ivory Coast ,  Ibrahima Fofana  tayari kabisa kufanya majaribio .
Azam FC kwasasa wapo kwenye mchakato wa kukifanyia marekebisho kikosi chake na moja ya eneo walilolimulika ni kuboresha eneo la ushambuliaji kwa kusajili washambuliaji wapya wawili wenye viwango vya juu.
Fofana (26), ametua nchini akitokea timu ya Union Sportive de Ben Guerdane ya Tunisia aliyokuwa akiichezea msimu uliopita uliomalizika Juni 14 mwaka huu.
Nyota huyo mwenye uwezo wa kucheza namba 9, 7 na 11, kabla ya kujiunga na timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Tunisia (Ligue 1) alikuwa akikipiga kwa miamba ya Ivory Coast Asec Mimosas tokea mwaka 2013 hadi 2015.
Fofana ataanza rasmi majaribio yake keshokutwa Ijumaa wakati kikosi cha Azam FC kitakapoendelea na mazoezi yake, ambapo kesho Alhamisi ni siku ya mapumziko.
Mshambuliaji huyo anaungana na makipa wawili wa kigeni, Daniel Yeboah (Ivory Coast) na Juan Jesus Gonzalez (Hispania), wanaoendelea kufanya majaribio ndani ya Azam FC wakigombea nafasi moja ya usajili ya golikipa.

Thursday, July 28, 2016

Kombe la dunia: Afrika kuongezwa nafasi 2 zaidi





Bara la Afrika litatunukiwa nafasi nyengine mbili zaidi iwapo dimba la dunia litaongeza idadi ya mataifa yanayoshiriki hadi 40 kuanzia mwaka 2026 kulingana na rais wa FIFA Gianni Infantino.
Infantino alipendekeza kuongezwa kwa timu hizo kabla ya kuchaguliwa kwake na shirikisho hilo la soka duniani.
Kwa sasa Afrika ina nafasi tano pekee katika michuano hiyo .
''Pendekezo langu limekuwa timu 40 na iwapo hilo litadhinishwa pendekezo langu ni kulipatia bara la Afrika nafasi mbili zaidi'',alisema Infantino.
Hatahivyo hatua hiyo itaidhinishwa hadi mwaka 2026 huku timu 32 zikiwa tayari zimethibitishwa kushiriki katika kombe la dunia la 2018 nchini Urusi na 2022 nchini Qatar.

Jamal Malinzi Apewa Sifa na FIFA




Rais wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Gianni Infantino amemsifu Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kuwa ni miongoni mwa viongozi wa vyama vya soka duniani walioamua kuendesha soka kwa weledi kutokana na kuratibu mafunzo mbalimbali kwa makocha na waamuzi.
Salamu za Infantino zimetolewa na Msimamizi Mkuu wa kozi ya waamuzi nchini, Carlos Henrique kutoka Afrika Kusini akisema, “Infantino ana ripoti zote ya namna mpira wa miguu unavyoendeshwa duniani. Anasifu Tanzania kwa  namna mnavyopiga hatua. Ana ripoti idadi ya makocha walivyokuwa wachache na sasa mna makocha wengine wako kwenye kozi.

“Mbali ya makocha, leo tuko nanyi waamuzi, ni hatua kubwa ambayo Rais Infantino amemsifu Rais wa TFF, Bwana Malinzi,” alisema Henrique.
Henrigue aliyeka waamuzi hao kujikita zaidi kusoma namna sheria 17 za mpira wa miguu zilivyoboreshwa kwa kuondoa zaidi ya maneno 1,000 ili kuja kusimamia vema michezo wa soka huku akiwataka kuwa mahiri wakati wote. Henrique anafanya kazi hiyo kwa kushirikiana na Mark Mzengo kutoka Malawi, Felix Tangawarima wa Zimbabwe na Gladys Onyago kutoka Kenya.
Kozi za Waamuzi wa Mpira wa Miguu wa Tanzania sasa ilianza  jana Julai 25, 2016 kwa waamuzi wenye Beji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (FIFA) na waaamuzi waandamizi wanaotarajiwa kuveshwa beji hizo kwa majina yao kupendekezwa FIFA kama watapata matokeo mazuri kwenye kozi inayoendelea.

Kozi ilianza kwa ratiba ya waamuzi wote kuchukuliwa vipimo (physical fitness test) kwa kila mwamuzi chini ya wakufunzi hao kutoka FIFA. Baada ya vipimo, darasa la waamuzi hao litaanza kwa nadharia na vitendo. Darasa hilo litafikia mwisho Julai 29, 2016 kabla ya kuanza darasa la waamuzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) na makamishna wa michezo kwa msimu wa 2016/2017.

Baada Ya Kutemwa Na Yanga, Salum Telela Je! Amesaini Mkataba Na Timu Nyingine Ya VPL




Kiungo wa zamani wa Yanga Salum Telela amesaini mtaba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu ya Ndanda FC ya mkoani Mtwara.
Telela amesaini mkataba huo leo mchana Julai 25, afisa habari wa klabu hiyo Idrisa Bandali ameiambia shaffihdauda.co.tz kuwa nyota huyo wa zamani wa Yanga amesaini rasmi mkataba wa mwaka mmoja kujiunga na klabu hiyo ya Kusini mwa Tanzania.
“Ni kweli Telela amesaini mkataba wa mwaka mmoja, lakini dau la usajili wake inabaki kuwa siri kati ya mwajiri na mwajiriwa kama yeye mwenyewe alivyotaka iwe,” alisema Bandali wakati nilipotaka athibitishe taarifa hizo kama ni za kweli au la.

Telela aliachwa na klabu ya Yanga baada ya mkataba wake kumalizika na kocha wa klabu hiyo Hans van Pluijm akasema nahodha huyo wa zamani wa timu za taifa za vijana hayuko katika mipango yake katika msimu ujao.

WAITWA STARS KUIKABILI NIGERIA. JEBA, MSUVA, MNYATE, KABUNDA NA WENGINE 20




Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania Charles Boniface Mkwasa ametangaza kikosi cha wachezaji 24 kitakachoingia kambini Julai 30 kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kimataifa dhidi ya Nigeria unatarajiwa kuchezwa mwanzoni mwa mwezi Septemba.
Mkwasa amesema ametoa nafasi kubwa kwa wachezaji vijana ili kuwapa uzoefu lakini ameongeza kuwa, atahitaji wachezaji wote kwasababu licha ya mechi hiyo kutokuwa na umuhimu wowote kwa timu zote mbili, lakini bado inaumuhimu linapokuja suala la kupanda katika viwango vya FIFA.
Kambi itaanza August 1-5 lakini wachezaji watatakiwa kuripoti kambini Julai 31 kwenye kambi ambayo itatajwa hapo baadaye
Wachezaji wote wa wanaocheza soka nje ya nchi wataungana na timu moja kwa moja Nigeria na baada ya mchezo huo watarejea tena kwenye vilabu vyao.
Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania kilichotangazwa kwa ajili ya kambi ambayo inatazamiwa kuanzia August 1 hadi 5 mwaka huu.
MAKIPA
Deogratius Munish, Beno Kakolanya (Yanga SC), Aishi Manula (Azam FC)
WALINZI
Oscar Joshua,  Kelvin Yondani, Juma Abdul (Yanga SC), Erasto Nyoni, Agrey Morris (Azam FC) Mohamed Hussein (Simba SC).
VIUNGO
Farid Musa, Himid Mao (Azam FC), Mohamed Ibrahim, Shiza Kichuya, Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude (Simba SC), Ibrahim Rajab ‘Jeba’ (Mtibwa Sugar FC), Hassan Kabunda (Mwadui FC), Simon Msuva, Juma Mahadh (Yanga SC).

WASHAMBULIAJI
Joseph Mahundi (Mbeya City), Ibrahim Ajib, Jamal Mnyate (Simba SC), John Bocco (Azam FC) na Jeremiah Juma (Tanzania Prisons).

Monday, June 20, 2016

Yanga Yaanza Vibaya Dhidi ya mo Bejaia fc






Mabingwa wa soka la Tanzania bara Yanga SC wameanza vibaya kampeni zao za kuwania kombe la Shirikisho Afrika baada ya kupoteza mchezo wao wa kwanza kwa bao 1-0 dhidi ya MO Bejaia ukiwa ni chezo wa Kundi A.
Yassin Sahli alifunga bao pekee kwenye mchezo huo na kuipa pointi tatu MO Bejaia iliyokuwa ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani Stade de I’Unite Maghrebine mjini Bejaia, Algeria.
Matokeo hayo yanaiacha Yanga katika nafasi ya tatu huku TP Mazembe wakiwa ndiyo vinara wa Kundi baada ya kushinda mchezo wao kwa magoli 3-0 dhidi ya Medeama ambayo inaburuza mkia.
Mazembe na MO Bejaia zinapointi sawa (pointi tatu) lakini TP Mazembe anaongoza kundi kwa tofauti ya magoli wakati Yanga na Medeama zikiwa hazina pointi lakini Yanga inakaa nafasi ya tatu kwa tofauti ya magoli. Medeama imefungwa magoli matatu wakati Yanga wameruhusu bao moja pekee.
Mchezo ujao wa Yanga utakuwa nyumbani (Dar es Salaam) June 28 itakapowaalika TP Mazembe kwenye uwanja wa taifa.

Sunday, June 19, 2016

Usajil Mpya Wa Arsenal wakamilika



Hikiwa Meneja Arsen wager Akijitaidi kuimarisha kikosa chake kwa ajili ya msimu ujao baada ya msimu uliopita kuandamwa vibaya na mashabiki kwa sababu ya matokeo mabaya
arsena imekamilisha dili la £3m la kinda wa naigeria  Kelechi Nwakali kwa dili la miaka 5 , Kelechi Nwakali nikiungo mwenye umri wa miaka 18 anacheza nafasi ya ukabaji  atayevalia namba 25 ndani ya jezi ya arsenal kwa msimu ujao.

Friday, June 17, 2016

Deal done Atletico Madrid






Atletico Madrid imethibitisha kuwa imekamilisha atua za mwazo za usajili wa  Nico  Gaitan kutoka benifica klabu hio imesama inasubiri kumalizika kwa mashindano ya copaamerica  na kumtangaza mchezaji huyo klabuni hapo.

Nico  Gaitan mwenye  umri wa miaka 28 anayekipiga katika klabu ya benifica akiwa ni raia wa argentina
 
kwa upande wake Nico Gaitan anaungana orodha ndefu ya wachezaji Benfica saini kutoka Amerika ya Kusini na kisha kuuzwa kwenye kwa faida kubwa ikiwa ni pamoja na Nemanja Matic, Fabio Coentrao, Ángel Di María, Javi García na Axel Witsel, ingawa hakuna bei imekuwa alitangaza kwa klabu ama bado.

Thursday, June 16, 2016

BREAKING NEWS: accidentally confirms Jamie Vardy move to Arsenal





England and Leicester Striker Jamie Vardy is highly linked to the Gunners this summer. According to various reports Jamie Vardy will decide his future after the Euros but BBC Sport have accidentally confirms his move to Arsenal.
Arsenal legend Robert Pires also believes Granit Xhaka and the potential signing of Jamie Vardy could help break his former side’s 12-year title drought in the Premier League.

arlier this month, the Gunners triggered Vardy’s £20million release clause at the King Power Stadium, which Leicester City boss Claudio Ranieri has since confirmed.

The 29-year-old forward is now believed to be mulling over a possible move to the Emirates while on England duty at Euro 2016 and Pires believes he has the ingredients the make it in north London.



Jamie Vardy is the striker Arsenal need to clinch the Premier league title. Jack Wilshere is also playing a big part in Vardy deal as he persuaded him to join the Gunners.

Tuesday, June 7, 2016

See How Tanzanian journalists use WhatsApp to report the news




In August of last year, Orton Kiishweko, a reporter with Tanzania’s Daily News, stumbled upon a story making the rounds on WhatsApp, the mobile messaging app.
“I read from a WhatsApp group that some Muslim Tanzanian clerics had been kidnapped by rebels in Eastern Congo and were demanding ransom,” Kiishweko recalls.
A bit of Googling corroborated the initial reports. But details were sketchy. So Kiishweko reached out to officials at the Ministry of Foreign Affairs to confirm the story. They provided him with the contact details of Tanzania’s ambassador to the Democratic Republic of the Congo (DRC). “I immediately saved the ambassador’s number on my smartphone and sent him a WhatsApp message,”
Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com