Thursday, August 18, 2016

Sasa Imetosha Kuwa na dada na kaka poa Kinondoni




Licha ya Serikali kuanzisha vita dhidi ya biashara haramu ya uuzaji mwili, Wilaya ya Kinondoni inakabiliwa na ongezeko la biashara haramu ya ngono kwa muda mrefu ambapo eneo la Tandale linatajwa kukithiri vibanda vingi vya dada na kaka poa.
Wakuu wa wilaya wengi wamepita katika wilaya ya Kinondoni pasipo kutokomeza changamoto hiyo. Lakini Mkuu wa sasa wa Wilaya hiyo Mh. Ally Hapi amejidhatiti kuuvunja mwiko huo. Hivi karibuni Hapi alitaja mikakati ya kutokomeza mtandao wa biashara hiyo.
Alisema atahakikisha anavunja vibanda vyote vinavyotumiwa na dada pamoja na Kala poa , vilevile watakaokamatwa watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Hapi alisema amepokea idadi ya vibanda vinavyotumiwa na dada poa na kwamba mpango wake ni kuvifunga kisha kutafuta wawekezaji ili Wamiliki wa vibanda hivyo walipwe fidia na kupisha ujenzi wa vitega uchumi.
“Niliwaagiza watendaji wa kata kuniletea idadi ya madanguro, nimeshajua mahali yalipo madanguro hayo, na kwamba nitakwenda kuchukua hatua ya kufunga madanguro pamoja na kuwapeleka dada poa mahakamani,” alisema. Alisema hatawachukulia hatua za kisheria dada/kaka poa pekee, bali hata wamiliki wa baa zitakazowahifadhi watu hao watachukuliwa hatua.
“Hatutashughulika na dada poa pekee bali hata Wamiliki wa nyumba na au baa watachukukiwa hatua. Hilo likitekelezwa
Kila mtu atatimiza wajibu wake, nimegundua wamiliki wengi wa madanguro hawapo hapa na idadi ya madanguro katika eneo la Tandale pekee kuna vibanda 58.” alisema.

Alisema utekelezaji wa ubomoaji nyumba umeshaanza kujadiliwa na kwamba wanasubiriwa wawekezaji ili wapewe fursa za kujenga maduka na vitega uchumi.
“Tunataka wenye fedha zao waje wawekeze ili tuwalipe fidia wenye nyumba, zibomolewe,” alisema na kuongeza.
“Huu mfupa uliwashinda watangulizi wangu lakini mimi nitautafuna.”
Kuhusu baa zinazokiuka sheria, alisema atawaondoa watendaji wa kata waliokaa muda mrefu kwa sababu wengi wao ndiyo chanzo cha ukiukwaji wa sheria.

“Watendaji waliokaa muda mrefu waondolewe sababu tumegundua hushirikiana na wenye baa kupiga kelele, wanachukua fedha zao na kuwaacha kupiga kelele usiku wa manane kinyume cha tarabibu,”

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com