Thursday, August 18, 2016

kijana wa miaka 16 anayetumia akili ya ziada kutengeneza pesa nyingi




Mwanafunzi wa Chuo Robert Mfune mwenye umri wa miaka 19, ameweza kutengeneza zaidi ya maelfu ya Paundi za Uingereza akiwa anafanyakazi katika muda wa ziada kwenye mgahawa ya McDonald’s kama mhudumu.
Robert ambae alipokua na umri wa miaka 16 tu, alianza kufanya kazi kama mhudumu katika kampuni ya McDonalds nyumbani kwao Southampton, ambako alipata kujifunza mambo mengi kuhusu biashara, na baadae kuanza kufanya biashara zake mwenyewe na kuweza kutengeneza pesa za kutosha kununua gari ya kifahari aina ya Bentley na kumnunulia nyumba ya kuishi mama yake mzazi.
Alisema ilikua ngumu sana kwake kufanya kazi katika mgahawa ya McDonald’s, kufanya biashara zake na kusoma kwa wakati mmoja.
“Nikama kwenda chuo na hela ya mkopo, kama utazingatia masomo na kuweka malengo ya kufanya vizuri basi utafanikiwa”. alisema mfanyabiashara Mfune. 
Mafanikio yake yalianza baada ya kumaliza masomo yake ya chuo, na kufanya kazi kama mhasibu katika idara ya fedha. Hivyo kumpelekea kupata ujuzi zaidi katika mambo ya biashara, na kuanza kufanya biashara zake akitumia akaunti zenye jina la mama yake na kuweza kupata mafanikio hayo.
“Nilipokua mhudumu nilijitahidi kujifunza mambo kazaa hivyo nikienda nyumbani nafanya utafiti mwenye na kufanya cha kwangu”. alisema Mfune.
Mfune kwa sasa anafanya biashara zake kwa kutumia akaunti yake mwenyewe, huku pia akiwa ameweza kuwekeza katika Migahawa ya chai mbalimbali mjini Uingereza.

Pia anamiliki magari yenye thamani ya zaidi ya Pauni 250,000£ ikiwemo Range Rover, Bentley continental GT ya rangi ya dhahabu lakini amedai kwamba yeye sio mtu wa kuthamini mali na magari bali utu wa watu na kujali marafiki zake.


0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com