kijana wa miaka 16 anayetumia akili ya ziada kutengeneza pesa nyingi
Mwanafunzi
 wa Chuo Robert Mfune mwenye umri wa miaka 19, ameweza kutengeneza zaidi
 ya maelfu ya Paundi za Uingereza akiwa anafanyakazi katika muda wa 
ziada kwenye mgahawa ya McDonald’s kama mhudumu.
Robert
 ambae alipokua na umri wa miaka 16 tu, alianza kufanya kazi kama 
mhudumu katika kampuni ya McDonalds nyumbani kwao Southampton, ambako 
alipata kujifunza mambo mengi kuhusu biashara, na baadae kuanza kufanya 
biashara zake mwenyewe na kuweza kutengeneza pesa za kutosha kununua 
gari ya kifahari aina ya Bentley na kumnunulia nyumba ya kuishi mama 
yake mzazi.
Alisema ilikua ngumu sana kwake kufanya kazi katika mgahawa ya McDonald’s, kufanya biashara zake na kusoma kwa wakati mmoja.
“Nikama
 kwenda chuo na hela ya mkopo, kama utazingatia masomo na kuweka malengo
 ya kufanya vizuri basi utafanikiwa”. alisema mfanyabiashara Mfune. 
Mafanikio
 yake yalianza baada ya kumaliza masomo yake ya chuo, na kufanya kazi 
kama mhasibu katika idara ya fedha. Hivyo kumpelekea kupata ujuzi zaidi 
katika mambo ya biashara, na kuanza kufanya biashara zake akitumia 
akaunti zenye jina la mama yake na kuweza kupata mafanikio hayo.
“Nilipokua
 mhudumu nilijitahidi kujifunza mambo kazaa hivyo nikienda nyumbani 
nafanya utafiti mwenye na kufanya cha kwangu”. alisema Mfune.
Mfune
 kwa sasa anafanya biashara zake kwa kutumia akaunti yake mwenyewe, huku
 pia akiwa ameweza kuwekeza katika Migahawa ya chai mbalimbali mjini 
Uingereza.
Pia
 anamiliki magari yenye thamani ya zaidi ya Pauni 250,000£ ikiwemo Range
 Rover, Bentley continental GT ya rangi ya dhahabu lakini amedai kwamba 
yeye sio mtu wa kuthamini mali na magari bali utu wa watu na kujali 
marafiki zake.

0 comments:
Post a Comment