Tuesday, January 3, 2017

Thomas Ulimwengu Kwenda Uholanzi


Klabu moja kutoka Uholanzi inatarajia kuleta ofa kesho ya kumuhitaji mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars),Thomas Ulimwengu.

Wakala wa Ulimwengu, Jamal Kisongo, amesema kwa sasa asingeweza kuitaja timu hiyo, hadi siku ya Jumatano, pamoja na ofa nyingine, zilizopo mezani hadi sasa.

Kisongo amesema kuna matarajio ya Ulimwengu kupata timu Ulaya na amewataka Watanzania wawe wavumilivu na kumuombea kijana huyo, ili afanikiwe kucheza Ulaya.

Ulimwengu, na Mbwana Samatta anayecheza Ubelgiji kwa sasa kwenye klabu ya Genk, tangu mwezi wa Januari mwaka uliopita, wote walikuwa wakiichezea TP Mazembe ya DR Congo kabla ya kumaliza mikataba yao mwaka uliopita. 

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com