Monday, November 14, 2016

Wasimamizi wa kazi za Prince wamezikataa Dola milioni 40 za Jay Z


Rapper Jay Z alituma barua ya maombi  kwa uongozi wa legend wa muziki Marekani  marehemu Prince, na kuomba umiliki wa nyimbo zake ambazo mpaka kifo chake alikuwa hajazitoa. Inasemekana Jay Z alitenga dola za kimarekani milioni 40 kwa ajili ya kukamilisha deal hilo.
Baada ya kuzungumza na uongozi wa Prince umekataa kusaini deal hilo na rapper huyo, ukidai kuwa Jay Z alishawahi kuziachia albamu 15 za Prince kwenye mtandao wake wa Tidal miezi michache tu baada ya Prince kufariki bila kibali chochote, na wanaamini Jay Z aliingiza pesa ndefu hivyo kuna uwezekano wa kumfungulia rapper huyo kesi ya madai.

Hata hivyo inasemekana uongozi unaosimamia kazi za Prince unafahamu Jay Z alikubaliana na Prince kuwa atasimamia albamu yake ya “HitNRun Phase One” ya mwaka 2015 lakini hakuna nyaraka za mikataba zinazoonyesha malipo ya dolla 750,000 ambazo ndio zilipaswa kulipwa ili kufunga mkataba.

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com