Monday, September 5, 2016

JE NGASA KUTUA BONGO ATARUHUSIWA KUSAJILIWA IKIWA DIRISHA LA USAJILI LIMEFUNGWA?





Baada ya Mrisho Ngasa kukanyaga ardhi ya Tanzania maswali kwa wadau wa soka yamekuwa ni kutaka kujua kama mchezaji huyo wa zamani wa Yanga ataruhusiwa kujiunga na klabu yoyote itakayomuhitaji.
Sports Extra ya Clouds ilimtafuta afisa habari wa TFF Alfred Lucas ili kujua taratibu na kanuni zikoje endapo kama kuna timu itataka kumsajili Ngasa kwa ajili ya michuano ya ligi kuu Tanzania bara lakini hata ikibidi mashindano ya kimataifa.

Lucas amesema Ngasa ananafasi ya kujiunga na timu yeyote itakayomuhitaji huku usajili huo ukitakiwa kufanywa kabla ya Septembre 6.
“Hata sisi tumeiona taarifa ya Ngasa kuwa hana mkataba tena na Free State Stars sasa kwa usajili wetu wa hapa nyumbani anaweza akapata nafasi kwasababu dirisha la usajili la FIFA linafungwa September 6 na hii lazima ieleweke vizuri sana, kilichofanya Yanga achelewe wakati ule ni usajili wa ndani kwa maana ya kwamba sisi TFF tulifungua usajili wa ndani kuanzia 15 June -16 August lakini kwa upande wa kimataifa dirisha linafungwa September 6”, Alfred Lucas alikaririwa na Clouds FM kupitia Sports Extra.
“Kwahiyo kama itatokea timu inamtaka kwasababu kama ameshapewa barua ya kuachwa kwaiyo inaweza ikamlinda kufdanyiwa  usajili.”
Ngasa amerejea Tanzania September 3 akitokea South Africa ambapo alivunja mkataba wake na klabu ya Free State Stars inayoshiriki ligi kuu nchini humo.

Baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa jijini Dar, Ngasa hakuwa tayari kuzungumza lolote juu ya kuvunja mkataba na kurejea nyumbai badala yake akasema: “Nimerudi nyumbani kwa sasa imi ni mchezaji huru nimekuja kupumzika kidogo kisha nitasema nitaenda kucheza wapi.”

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com