Monday, August 22, 2016

SERENGETI BOYS YAZIDI KULETA MATUMAINI YA KUELEKEA MADAGASCAR




Timu ya taifa ya vijana chini miaka 17 ‘Serengeti Boys’ imepata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya timu ya vijana ya Afrika Kusuni katika mchezo wa marudiano uliochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex kuwania kufuzu fainali za matifa ya Afrika kwa vijana wa umri huo mashindano yanayotarajiwa kufanyika Madagascar.
Magoli ya Serengeti Boys yamefungwa na kipindi Mohamed Abdala aliyefunga dakika ya 34 kipindi cha kwanza wakati bao la pili likifungwa dakika za lala salama na Muhsin Makame.
Serengeti Boys imeitupa nje timu ya taifa ya Afrika Kusini kwa jumla ya magoli 3-1 hiyo ni baada ya timu hizo kutoka sare ya kufungana 1-1 kwenye mchezo wa awali uliopigwa Afrika Kusini.

Matokeo hayo yanaifanya Serengeti Boys isonge mbele, itakutana na Namibia au Congo Brazzaville katika raundi inayofuata na endapo itafanikiwa kufuzu basi itakata tiketi ya kushiki katika fainali za mataifa ya Afrika.
Ally Ng’anzi wa Serengeti Boys alioneshwa kadi nyekundu kwenye mchezo huo baada ya kuoneshwa kadi mbili za njano hivyo ataukosa mchezo mmoja ujao wa timu yake.

September mwaka huu Serengeti itakuwa mwenyeji wa Namibia au Congo Brazzaville huku mchezo wa marudiano ukitarajiwa kuwa kupigwa mwezi October.

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com