Saturday, October 17, 2015

Mbunge afariki katika ajali ya ndege Tanzania

Deo Filikunjombe
 Mbunge wa eneo la Ludewa aliyekuwa anamaliza muda wake, amefariki kwenye ajali ya ndege iliyotokea Alhamisi.
Bw Deo Filikunjombe alikuwa safarini kutoka jiji la Dar es Salaam kuelekea jimbo lake la Ludewa ajali ilipotokea.
Alikuwa miongoni mwa abiria wanne kwenye ndege hiyo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda (Mb) anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge anayemaliza muda wake (Jimbo la Ludewa) Mhe. Deo Filikunjombe, kilichotokea jana kwa ajali ya Ndege (Helicopter).
“Ajali hiyo ... ilitokea jana jioni tarehe 15 Oktoba, 2015 wakati Helicopter waliyokuwa wakisafiria kutokea Jijini Dar es Salaam kuelekea Jimboni kwake Ludewa kuanguka katika Hifadhi ya Selous Maeneo ya Msolwa Mkoani Morogoro,” unasema ujumbe uliowekwa kwenye tovuti ya bunge la nchi hiyo kutangaza kifo chake.
Bw Filikunjombe alizaliwa mwaka 1972 na alichaguliwa mbunge wa eneo la Ludewa lililoko mkoani Njombe mwaka 2010.

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com