Tuesday, August 16, 2016

MASHABIKI KUZOMEA BAADA YA FILIMBI YA MWISHO




Thierry Henry amewatetea washabiki wa Arsenal ambao walizomea timu yao baada ya mchezo dhidi ya Liverpool kumalizika.
Arsenal wamepoteza kwa mabao 4-3 dhidi ya Liverpool baada ya kuruhusu mabao manne ya haraka chini ya dakika 20.
Na mwamauzi wa mchezo huo Michael Oliver alilpopuliza filimbi ya mwisho tu, washabiki wote waligeuka na kuanza kuzomea timu yao.
Arsenal wameshinda mara moja tu michezo ya ufunguzi wa ligi ya England tangu kuingia kwa muongo mpya, na sasa washabiki wa klabu hiyo wanazidi kukatishwa tamaa.
“Washabiki hawakuwazomea wakati wako nyuma kwa 4-1, waliisapoti timu,” alisema Henry kwenye runinga ya Sky Sports. “Lakini baada ya mchezo walikereka na ndiyo maana walizomea.

“Kuna vitu vingi sana vya kuangalia, lakini kikubwa zaidi ni kupoteza nyumbani kwa mara nyingine tena.”

Jamie Redknapp aliongeza: “Sina huruma na Wenger hata kidogo, nadhani vijana wamefanya vyema lakini hawakupaswa kuchezeshwa kwenye mchezo kama ule.
“Unaweza kumpa Giroud dakika 10, Koscielny pia…naamini Payet atacheza kwa upande wa West Ham kesho (leo) .”

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com