MBWAA KUTOKA MAREKANI WA UKAGUZI WAWASILI DAR..
Ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam unawakaribisha
wanachama wapya wa timu ya mbwa maalumu wa ukaguzi (Canine Detection Team
Tanzania) #CanineDetectTZ Katika
kipindi cha kiangazi cha mwaka jana maafisa wa polisi wa Kitanzania wanne
walikwenda nchini Marekani kwa ajili ya mafunzo maalum katika Chuo cha Idara ya
Forodha na Ulinzi wa Mipaka ya Marekani jijini El Paso huko Texas. Katika mafunzo
hayo maafisa hao pamoja na mbwa wao walipewa mafunzo ya kubaini bidhaa
zitokanazo na wanyama pori zinazovushwa kimagendo na madawa ya kulevya. Maafisa
hao na mbwa wao waliungana tena jijini Dar es Salaam wiki iliyopita kwa ajili
ya mafunzo kwa vitendo katika eneo lao la kazi. Fuatilia ukurasa wetu wa
Facebook katika wiki zijazo ili kufahamu Zaidi kuhusu mbwa hao na programu hii
mpya!
0 comments:
Post a Comment