Featured
Showing posts with label sport. Show all posts
Showing posts with label sport. Show all posts

Wednesday, November 23, 2016

Manchester United yamtamani Nyota wa Genk, mwenyewe awatahadharisha


Imeripotiwa kuwa Manchester United imetuma watu wake kwa ajili ya kumfuatilia winga chipukizi wa Genk ya Ubelgiji, Leon Bailey ili kumsajili baada ya msimu wa 2016/2017 kumalizika mwakani.
Inasemekana kuwa Man United inavutiwa na uwezo wa winga huyo mwenye miaka 19 na ipo tayari kumsajili ili kujiunga na kikosi cha klabu hiyo kinachonolewa na Mreno, Jose Mourinho.

Akizungumza kuhusu Man United kutaka kumsajili, Bailey alisema ana ndoto za kucheza Ligi Kuu ya Uingereza lakini kama Manchester United itashindwa kumthibitishia namba katika kikosi cha kwanza basi hatajiunga.


“Ninandoto za kucheza Ligi Kuu ya Uingereza, lakini kama Man United itanipangia dakika za kucheza, nitabaki Genk,” alisema Bailey.

WACHEZAJI wa Zesco United, kiungo Misheck Chaila na mshambuliaji Jesse Were wamesema kwamba hawajazungumza na Yanga SC juu ya mpango wa kumfuata kocha wao, George Lwandamina aliyetangulia kwa mabingwa hao wa Tanzania.


Tovuti ya Supersport imeandika kwamba mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya na kiungo wa Zambia wameripotiwa kuwa mbioni kujiunga na vigogo wa Tanzania katika dirisha hili la majira ya baridi kumfuata Lwandamina.

Were, ambaye amefunga mabao 15 katika msimu wake wa kwanza wa Zesco, kufuatia kujiunga na wababe hao wa Zambia kutoka Tusker ya kwao, Kenya Januari, amesema yeye 'bado yupo yupo' sana Zesco.

"Yote nayoweza kuzungumza kuhusu sakata la Yanga ni kwamba hawajazungumza na mimi. Kumekuwa na tetesi juu ya hili ndiyo, na nimesoma juu ya hili,” alisema Were.

Pamoja na hayo, Were amesema kwamba mpira upo miguuni mwa Zesco, kukubali au kukataa ofa ya Yanga ikitokea wakatuma maombi ya huduma zake.

"Lakini kwa sasa mimi ni mchezaji wa Zesco, nina mkataba, nina furaha, fikra zangu zipo kwenye mechi zilizosalia na nipo tayari kuwa hapa hadi nimmalize mkataba wangu mwishoni mwa msimu wa 2017,” alisema Were.

Kwa upende wake, Chaila amekanusha pia kufanya mazongumzo na Yanga au Lwandamina jus ya kujiunga na mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania.

“Hakuna hate momma aliyezungumza na mimi au klabu. Zote ni tetesi tu,” alisema Chaila. “Hakika sijazungumza naye (Lwandamina) tangu aondoke, lakini namuheshimu kama mzazi wangu,".”

Jesse Were amesema Zesco ndiyo wenye maamuzi iwapo Yanga watatuma maombi ya kutaka huduma zake


Saturday, November 19, 2016

LANGA LESSE BERCY WA KONGO - BRAZZAVILLE AINGIA MITINI VIPIMO VYA UMRI CAF


MCHEZAJI wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Kongo- Brazzaville, Langa Lesse Bercy ameshindwa kuwasili Cairo, Misri kwa ajili ya kufanyiwa vipimo na uchunguzi juu ya umri wake kama alivyotakiwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilimkatia Rufaa CAF Langa Lesse Bercy baada ya kujiridhisha amevuka umri wa kucheza mashindano ya U-17.
Na hiyo ilifuatia Kongo- Brazzaville kuitoa Tanzania, Serengeti Boys katika hatua ya mwisho ya mchujo wa kuwania fainali za U-17 Afrika mwakani nchini Madagascar. 


Kutokana na rufaa hiyo, Langa Lesse Bercy alitakiwa na CAF kufika makao makuu ya shirikisho hilo, Cairo, Misri kwa ajili ya kurudia na kuthibitisha umri wake kwa kipimo cha MRI (Magnetic Imaging Resonance).
Na TFF ilikubali sharti la CAF kugharamia zoezi zima ikiwa ni pamoja na kulipia gharama za usafiri wa mchezaji husika na daktari wake  pamoja na kulipia gharama za vipimo.


Wakati zoezi la vipimo limepangwa kufanyika leo, Shirikisho la Soka la Kongo- Brazzaville limetoa taarifa kwamba Langa Lesse Bercy hataweza kutokea kwa sababu ambazo ziko nje ya uwezo wao.
Zoezi limepangwa kufanyika leo kuanzia Saa 5.00 asubuhi mjini Cairo, Misri. Ujumbe wa TFF wa watu wanne ukiambatana na madaktari wawili uliwasili mjini Cairo tangu Novemba 17, 2016 ili kuwa shuhuda wa zoezi la kipimo hicho.
Na jana usiku saa 5.00 TFF ilipokea ujumbe kutoka CAF kuwa mchezaji Langa Bercy ameshindwa kusafiri kwenda Cairo kwa kuwa yuko katika eneo lililoko "vitani",eneo hilo halikutajwa.
Taarifa ya TFF kwa vyombo vya Habari leo, imesema kwamba wanaendelea kufuatilia kwa karibu jambo hili ili kuhakikisha haki inatendeka .

Thursday, November 17, 2016

SIKILIZA ASICHOSEMA MGHANA WA AZAM BAADA USAJILI


NYOTA mpya wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Yahaya Mohammed, amesema kuwa amejiunga na timu hiyo kwa kazi moja tu kuipigania timu ili kupata matokeo bora uwanjani.
Mohammed jana jioni alikamilisha usajili wa kujiunga na timu hiyo akisaini mkataba wa miaka miwili tayari kabisa kuitumikia Azam FC kuanzia mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), Kombe la Kagame ikiwa kama bingwa mtetezi, Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) na Kombe la Shirikisho Afrika mwakani.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Aduana Stars ya Ghana, 28, ameuambia mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz kuwa mashabiki wa Azam FC wake mkao wa kufurahi kwani kwa kushirikiana na wachezaji wenzake watafanikiwa kuwapa furaha kwa kupata matokeo bora uwanjani.
“Ninafuraha kubwa kusaini mkataba wa kujiunga na Azam FC, nimejipanga kukabiliana na changamoto zote hapa kwani ukiwa mchezaji ni kazi yako na unapaswa kujiandaa na hilo na kila muda unapaswa kujiandaa na kazi yako,” alisema.
Staa huyo pia alichukua fursa hiyo kuomba sapoti kwa mashabiki wa timu hiyo, waendelee kuisapoti Azam FC kwani hilo litawapa nguvu wao kama wachezaji kuweza kufanya vizuri uwanjani na kupambana kwa ajili ya matokeo bora.
“Tunahitaji sapoti yao na waendelee kuipa sapoti Azam FC, hilo litatufanya sisi kuipeleka timu mbele zaidi, sisi pekee wachezaji hatuwezi kuipeleka timu mbele kama mashabiki hawatusapoti, tunawahitaji sana na sisi wanatuhitaji, waisapoti timu katika hali mbaya na nzuri kwani hii ni timu yao, sisi tutaingia uwanjani kucheza kwa ajili yao na tunawaahidi tutawapa furaha kwa matokeo mazuri,” alisema.
Akizungumzia kuhusu soka la Tanzania, aliongeza kuwa: “Kwa sasa sijui lolote kuhusu soka la Tanzania kwani nikiwa Ghana hakuna kituo cha televisheni kinachoonesha ligi ya hapa, ila kwa sasa mimi ni mwanafamilia wa Azam FC, hilo sio tatizo kwangu ukiwa kama mchezaji unatakiwa kusimama popote na kucheza na kufanya vizuri kwa ajili ya klabu.”
Straika huyo anatarajia kuanza rasmi mazoezi Desemba 3 mwaka huu, wakati kikosi hicho kitakaporejea kutoka likizo ya wiki mbili, ambapo kesho Ijumaa atarejea nchini kwao Ghana kwa ajili ya kujipanga zaidi pamoja na mapumziko mafupi.
Mbali na kuiongoza Aduana Stars kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Ghana msimu uliopita, Mohammed pia aliiibuka mfungaji bora namba mbili wa ligi hiyo kwa mabao 15 aliyofunga nyuma ya Latif Blessing wa Liberty Proffesional aliyetupia 17.
Mohammed alikuwemo kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Ghana kilichoshiriki fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) zilizofanyika mwaka juzi nchini Afrika Kusini na timu hiyo kuwa washindi wa pili akiwa pamoja na straika mwingine aliyesajiliwa na Azam FC, Samuel Afful.

Wednesday, November 16, 2016

SIMBA SC YAKUBALI KUTOA SH MILIONI 240 KUREJESHEWA OKWI


SIMBA SC imekubali kulipa dola za Kimarekani 120,000, zaidi ya Sh. Milioni 240 kwa klabu ya Sonderjiske ya Denmark ili kurejeshewa mshambuliaji wake, Mganda Emmanuel Okwi.

Na baada ya Simba SC kulipa fedha hizo, Okwi atarejea kufanya kazi Msimbazi kwa mkataba wa mwaka mmoja kwa mujibu wa makubaliano hayo.
Simba SC ilimuuza Okwi kwa dola 100,000 mwaka juzi Denmark, lakini kutokana na mchezaji huyo kutopata nafasi ya kucheza Ulaya, inaamua kumrejesha na makubaliano yamefikiwa.


Dola 120,000 tu wale jamaa wanataka watuachie Okwi. Na Okwi naye atasaini kwa mshahara tu mkataba wa mwaka huu, hatumpi dau la kusaini yeye,"kimesema chanzo kutoka Simba.  

Okwi ni mchezaji aliyeipa faida kubwa Simba ndani na nje ya Uwanja enzi zake anacheza Msimbazi. Mbali na kuwasaidia Wekundu wa Msimbazi kushinda matajii mbalimbali tangu ajiunge nao kwa mara ya kwanza mwaka 2010, Okwi pia ameinufaisha kifedha Simba SC.
Simba ilimuuza Okwi Etoile du Sahel ya Tunisia Januari mwaka 2013 kwa dau la rekodi kwa klabu za Tanzania, dola 300,000, ingawa baada ya muda akaingia kwenye mgogoro na klabu hiyo ya Tunisia.


Mtafaruku ulianza baada ya Okwi kuchelewa kurejea mjini Sousse mkoani Sahel baada ya ruhusa ya kwenda kuichezea timu yake ya taifa, Uganda.
Okwi naye akadai Etoile walikuwa hawamlipi mishahara na kufungua kesi FIFA (Shirikisho la Soka la Kimataifa), ambayo mwisho wa siku alishinda kwa kuruhusiwa kutafuta timu nyingine ya kuchezea kulinda kipaji chake, wakati wa mgogoro wake na klabu ya Tunisia.
Okwi akajiunga na SC Villa ya kwao, Kampala katikati ya mwaka 2013 na Desemba mwaka huo, akahamia Yanga SC.


Hata hivyo, Okwi akavunja Mkataba na Yanga SC Agosti waka 2014, baada ya timu hiyo ya Jangwani kushindwa kumlipa dola za Kimarekani 60,000 kama ilivyokuwa katika Mkataba baina yao na kurejea klabu yake ya zamani, Simba.

Na mapema Oktoba mwaka 2014, Simba SC nayo ilimuuza Okwi  SonderjyskE FC ya Ligi Kuu ya Denmark ambako alisaini Mkataba wa miaka mitano.
Akiwa katika mwaka wa pili wa Mkataba wake wa miaka mitano, Okwi anatarajiwa kurejea Simba tena.

Seongam na Serengeti Boys za Toshana Nguvu



Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 Serengeti Boys, jana imelazimisha sare ya bila kufungana na wenyeji Seongnam FC katika ziara yake ya Korea Kusini.
Serengeti ambayo iko huko kwa mwaliko wa Shirikisho la Soka la Korea Kusini, itarejea wiki ijayo na kucheza mchezo mwingine wa dhidi ya nyota 40 walioteuliwa na Airtel baada ya michuano ya Kampuni hiyo ya simu.
Serengeti Boys imepata nafasi hiyo kutokana na umahiri wake wa kucheza soka la ushindani kwani kwa kipindi cha mwaka mmoja tu, imeweza kucheza michezo 16 ya kimataifa ambako imekuwa ikifanya vema katika mechi 15 kabla ya 16 iliyopoteza dhidi ya Congo-Brazaville katika michuano ya kuwania nafasi ya kucheza Kombe la Mataifa ya Afrika.

AZAM FC YASAJILI NYOTA WAWILILI


UONGOZI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, unayofuraha kuwaataarifu wapenzi wa soka kuwa jioni ya leo umefanikiwa kuingia mikataba na wasshambuliaji nyota kutoka Ghana, Samuel Afful na Yahaya Mohammed.

Zoezi la kuingiana mikataba limehudhuria na baadhi ya viongozi wakuu wa timu wakiwemo Ofisa Mtendaji Mkuu, Saad Kawemba, Meneja Mkuu, Abdul Mohamed, Kocha Mkuu Zeben Hernandez pamoja na wakala anayewasimamia wachezaji hao, Kingsley Atakorah, ambaye pia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Adom Wonders Academy ya nchini Ghana.

Wakati Afful, 20, akisaini mkataba wa miaka mitatu, Mohammed aliyetua nchini leo mchana akitokea Ghana naye amesaini kandarasi ya miaka miwili tayari kabisa kuanza kuitumikia timu hiyo yenye maskani yake Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Afful ambaye mpaka sasa yumo katika vikosi vya timu za vijana za Ghana chini ya umri wa miaka 20 na 23, anajiunga Azam FC akitokea timu ya Sekondi Hasaacan ya Ghana, ambayo aliifungia mabao tisa timu hiyo msimu uliopita.

Moja ya rekodi yake ni kuifungia bao muhimu timu ya Taifa ya Ghana chini ya umri wa miaka 20 (U-20) mwaka jana dhidi ya Zambia kwenye ushindi wa mabao 2-1, lililoipa nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia nchini New Zealand, baada ya kutinga nusu fainali ya Mataifa ya Afrika kwa Vijana (U-20) zilizofanyika Senegal mwaka jana.

Mohammed ambaye ni mshambuliaji mzoefu anayetokea Aduana Stars, alikuwa ni mfungaji bora namba mbili wa Ligi Kuu ya Ghana msimu uliopita akifunga mabao 15, pungufu ya mabao mawili na kinara Latif Blessing (Liberty Proffessional) aliyetupia 17.

Azam FC tunaamini ya kuwa ujio wa nyota hao, utazidi kuipa nguvu timu yetu kuelekea kwenye michuano inayotukabili mbeleni, mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Kombe la Kagame (CECAFA Kagame Cup) tukiwa kama mabingwa watetezi, Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) na Kombe la Shirkisho Afrika (CC) mwakani.

Azam FC tunapenda kuwafahamisha mashabiki wetu kuwa tutaendelea kuyafanyia kazi mapendekezo ya benchi la ufundi kwa kukifanyia marekebisho kikosi chetu katika usajili huu wa dirisha dogo uliofunguliwa jana, lengo ni kukipa nguvu zaidi kikosi chetu bili kifanye vizuri zaidi katika michuano ya hapa nchini pamoja na ile ya Kimataifa.


Azam FC itaendelea kuwathamini mashabiki wake na tunaamini ya kuwa uwepo wenu utaendelea kutupa nguvu zaidi katika mapambano yetu makubwa ya kila siku na yaliyoko mbele yetu, tunachowaahidi ni kuendelea kuwapa furaha zaidi kwa kupata matokeo bora uwanjani na tunawaomba muendelee kuwa pamoja nasi.

Monday, November 14, 2016

Pascal Wawa kutimkia El Emerreikh inchini Sudan



Beki wa kati wa kimataifa wa Ivory Coast aliyekuwa anaichezea klabu ya Azam FC ya Dar es Slaam Tanzania Pascal Wawa, leo November 14 2016 habari zilizoenea katika mitandao ya kijamii kuhusu beki huyo ni kuwa amesaini El Emerreikh ya Sudan.
Wawa ameamua kurudi El Merreikh ya Sudan kwa kusaini mkataba wa miaka miwili wa kutumikia klabu hiyo, ambayo awali aliwahi kuichezea kwa kipindi cha miaka minne.

Pascal Wawa alijiunga na Azam FC mwaka 2014 akitokea klabu ya El Marreikh ya Sudan mwaka, na amefanikiwa  kuichezea Azam FC katika kipindi cha misimu miwili.

Sikiliza madudu ya Kocha Mkuu wa Taifa Satrs Baada ya Kupewa kichapo....




Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Charles Boniface Mkwasa amesema timu yake imepoteza kwa bahati mbaya mchezo dhidi ya Zimbabwe huku akitaja magoli mawili ya haraka ya kipindi cha kwanza na kipindi cha pili kuchangia kufanya mchezo kuwa mgumu kwao.
Taifa Stars imepoteza mchezo wake wa kirafiki wa kimataifa kwa kipigo cha magoli 3-0 ugenini dhidi ya wenyeji Zimbabwe.

Tanzania ilisafiri kuelekea mjini Harare ikiwa na nyota wake wote wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi pamoja na wale wanaocheza ligi ya ndani kucheza mchezo wa kirafiki uliopo kwenye kalenda ya FIFA. Mchezo huo ulikuwa na faida kwa Tanzania kujipandisha kwenye viwango vya FIFA kwama Stars ingepata ushindi.
Kwa upande wa Zimbabwe mchezo huo wameutumia kujipima wakati huu wakijiandaa kucheza fainali za mataifa ya Afrika (AFCON 2017) zinazotarajiwa kufanyika Gabon.

Magoli ya Zimbabwe yamefungwa na Knowledge Musona dakika ya 9, Mathew Rusike dakika ya 55 na Nyasha Mushekwi dakika ya 57.

Stars ilipata nafasi kadhaa za kufunga lakini haikufanikiwa kukwamisha mpira kambani. Mwana Samatta alipata nafasi ya kufunga lakini shuti lake liliokolewa na golikipa wa Zimbabwe kabla ya mpira wa kichwa uliopigwa na Elias Maguli kuokolewa na golikipa huyo aliyecheza kwa kiwango cha juu.
Baada ya mchezo kumalizika, kituo kimoja cha habari kilifanya mazungumzo moja kwa moja na afisa habari wa TFF Alfred Lucas ili kujua kocha wa Taifa Stars Boniface Mkwasa amepokeaje matokeo hayo pamoja na kutaja sababu ya timu yake kupoteza mchezo.

Kwa mujibu wa Alfred Lucas, Mkwasa amesema Stars imepoteza mchezo kwa bahati mbaya lakini aina ya magoli waliyofungwa yaliwachanganya wachezaji.

“Kocha amesema timu imepoteza mchezo kwa bahati mbaya lakini amesema, aina ya magoli yalifyofungwa yaliwachanganya wachezaji na kupelekea kupoteza mchezo. Amesema Zimbabwe ilifunga goli la mapema kipindi cha kwanza (dakika ya 9) ambalo liliwachanganya wachezaji na muda mwingi wakawa wanafikiria zaidi kusawazisha,” amesema Lucas akinukuu maneno ya Mkwasa baada ya mechi.
“Kipindi cha pili wakati Stars ikijipanga kusawazisha, ikafungwa tena goli la mapema (dakika ya 55) na kuvuruga mipango yao ya kuhakikisha wanasawazisha.”

Kwa mujibu wa Alfred Lucas, Stars inatarajia kurejea nchini kesho saa 3 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Saturday, November 5, 2016

CAF wamekiita kijeba cha Congo Brazzaville wakipime umri



Shirikisho la soka barani Africa (Confederation of African Football) lipo mbioni kufanya uchunguzi kufatia madai ya Congo fanya udanganyifu kwa mumchezesha mchezaji anayedhaniwa kuvuka umri kwenye mechi za kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wa U17.

Congo-Brazzaville imefanikiwa kufuzu fainali hizo zitakazofanya mwaka ujao huko Madagascar baada ya kuiondosha Tanzania raundi ya mwisho ya kuwania kufuzu.

Laikini Tanzania ilipeleka malalamiko yake ikidai wapinzani wao kutumia wachezaji waliovuka umri uliowekwa na Caf kwenye mashindano husuka.

Shirikisho la soka Tanzania (TFF) liliindikia Caf likitaka wachezaji wanaolalamikiwa kuvuka umri wafanyiwe vipimo vya kuhakiki umri wao.

Kwa upande wao Caf wamemtaja mchezaji mmoja Langa-Lesse Bercy kwa ajili ya kumfanyia vipimo kwasababu Namibia (litolewa na Congo) waliwahi kulalamikia umri wa mchezaji huyo.

Mkurugenzi wa tiba wa Caf Dr Boubakary Sidiki amethibitisha kwa kuiandikia barua TFF kwamba, Bercy ambaye alifunga magoli dhidi ya Namibia na Tanzania na kuisaidia nchi yake kufuzu, atafanyiwa vipimo November 18 jijini Cairo, Misri.

Bercy atasafiri hadi Misri aiambatana na daktari wake wakati TFF pia watatuma madaktari wao kwa ajili ya kushuhudia zoezi hilo la upimwaji wa mchezaji anayelalamikiwa.
TFF pia watalipia gharama zote zitakazohitajikana Caf.

Kwa mujibu wa kanuni za Caf, udanganyifu wa umri ni kosa ambalo linapelekea nchi husika kufungiwa miaka mitatu kushiriki mashindano ya umri husika.

Nchi nne zitakazofanikiwa kucheza nusu fainali ya mashindano hayo, zitakuwa zimefuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia chini ya miaka 17 zitakazofanyika India.

Sunday, October 30, 2016

Bondia Mtanzania amchakaza makonde mwenzake wa China




Bondia chipukizi kutoka Tanzania Abdallah Pazi Dulla Mbabe alimrambisha sakafu mwenzake kutoka China Zheng Chengbo katika pigano kali lililofanyika usiku wa Ijumaa katika ukumbi wa Diamond Jubilee mjini Dar es Salaam.

kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania ngumi nzito iliorushwa na Dulla ilimwangusha mpinzani wake na kumfanya kushindwa kuendelea na pigano hilo la uzani wa Light Heavy.

Pazi alianza pigano hilo kwa kasi na kufanikiwa kumwangusha bondia huyo wa China kwa sekunde kadhaa.
Hatahivyo Chengbo aliamka na kuendelea na pigano.
The Citizen linasema kuwa bondia huyo wa Tanzania alifanikiwa kumweka Chengbo katika kona na kumrushia makonde makali akimwacha akitokwa na damu chungu nzima katika pua.

Ni wakati huohuo ambapo bondia huyo alishindwa kunyanyuka kutoka sakafuni ndiposa refa akamaliza pigano hilo na kumpatia ushindi wa Knock-out Dulla.

Bondia huyo sasa ameshinda mapigano 14 ,13 yakiwa katika njia ya Knockout na kushindwa mara tatu.

Thursday, October 27, 2016

Wakala wa Farid Musa akanusha kupatikana kibali cha kazi, mchakato bado unaendelea




UONGOZI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, unapenda kuwataarifa wapenzi wa soka kuwa winga wao Farid Mussa, leo amepata kibali rasmi cha kufanya kazi nchini Hispania.
Kwa muda mrefu Azam FC imekuwa ikisubiria kibali hicho ili mchezaji huyo akaanze maisha mapya ya soka nchini humo katika timu ya Deportivo Tenerife inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza.
Kufuatia kibali hicho kupatikana, Mussa anatarajia kuondoka nchini muda wowote kuanzia sasa kwenda kuitumikia timu hiyo.
Tunapenda mashabiki wa soka watambue kuwa Mussa anakwenda Tenerife kwa kwa makubaliano maalumu ya pande zote mbili ukiwa ni usajili wa mkopo na Azam FC itanufaika kupitia uhamisho wake mwingine atakaposajiliwa kwenda timu nyingine barani humo.
Tunaamini uwepo wake kwenye klabu hiyo utafanikisha kukuza kipaji chake zaidi pamoja na thamani yake kwa ujumla, ukizingatia bado ni mchezaji kijana anayeendelea kujifunza.
Kabla ya kibali hicho kutoka, kuna taarifa mbalimbali zilizotolewa zikiihusisha Azam FC kuwa tumemzuia kijana wetu huyo kujiunga na timu hiyo, lakini inaomba ieleweke kuwa kibali kilichotolewa leo hii ndicho kilichokuwa kikikwamisha uhamisho huo na tunamshukuru Mungu kimepatikana.

Tunaomba ieleweke kuwa, Azam FC haitafanya jitihada zozote za kuziba milango ya wachezaji wetu pindi watakapopata timu nje ya nchi, sisi tutakuwa wa kwanza kuwaongoza katika kufikia malengo yao makubwa ya kucheza soka la kulipwa kwenye maslahi mazuri endapo taratibu za usajili zitafuatwa.
Azam FC tunapenda kuishukuru Tenerife kwa kufanikisha uhamisho huo na tunamtakia mafanikio mema Mussa katika maisha yake mapya ya soka na tunaamini ataitangaza vilivyo timu yetu kimataifa na Tanzania kwa ujumla jambo ambalo litafungua milango kwa wachezaji wengine kuungana naye huko.

Imetolewa na Uongozi wa Azam FC

Jana usiku Azam TV kupitia kipindi cha MSHIKEMSHIKE VIWANJANI walithibisha kupatikana kwa kibali cha kazi cha kiajana Farid Musa kwa ajili ya kwenda kucheza soka la kulipwa kwenye klabu ya Tenerife ya nchini Hispania, lakini General Manager wa Azam FC Abdul Mohamed alisikika kwenye radio akithibisha kupokea kibali cha kazi cha winga huyo ambaye kwa sasa hajacheza mechi yoyote ya kiushindani tangu kuanza kwa ligi akisubiri safari yake kuelea Ulaya.

Wakala wa Farid Musa, John Sorzano amekanusha habari zilizozagaa kuwa tayari kibali cha kazi kimeshatoka na badala yake amesema hicho kilichotapakaa kwenye mitandao ya kijamii si kibali ni form ambayo itatumiwa katika mchakato wa kuombea kibali.
Solzano ameshangaa form hiyo kutapakaa mitandaoni wakati ni kitu cha siri huku akisisitiza kuwa, wametumiwa Azam na yeye lakini kwa upande wa Tanzania, tayari form hiyo imeshaonekana kwenye mitandao ya kijamii. Kitendo cha hiyo form kusambaa mitandaoni huenda kukahatarisha Farid kupata kibali cha kazi.
“Hii form nimetumiwa mimi pamoja na klabu ya Azam, lakini nashangaa wao wameiweka mitandaoni wakati ni kitu cha siri, kwa upande wangu mimi nilifanya kuwa siri. Farid sio kwamba amepata kibali lakini mchakato bado unaendelea,” anasema John Sorzano wakala wa Farid Musa.

“Kitendo cha kuitoa form hadharani ambayo ni document ya serikali kinaweza kikahatarisha mchakato kwasababu ikumbukwe Tanzania pia kuna ubalozi wa Hispania ambao unaweza kuona yanayofanyika kwenye mitandao ya kijamii wanaweza wakahoji kwanini document hiyo imesambaa hivyo, inaweza kuleta ugumu.”

Monday, October 24, 2016

Hans van Pluijm amejiuzulu Yanga baada ya kusikia ujio wa kocha mpya




Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga Hans van der Pluijm ameandika barua ya kujiuzulu kuifundisha klabu hiyo ya Jangwani.

Uamuzi wa Pluijm umekuja baada ya tetesi kuzangaa kwamba uongozi wa klabu hiyo unampango wa kubadili benchi la ufundi la klabu hiyo huku yeye kama kocha wa sasa akiwa hana taarifa rasmi kutoka kwa klabu.

“Nimeandika barua ya kujiuzulu kutokana na jinsi mambo yanavyokwenda, sikufurahishwa nayo. Nimeamua kujiuzulu na tayari nimekabidhi barua kwa uongozi wa Yanga, kama watapitisha nahitaji wanikamilishie stahiki zangu,” Van Pluijm amenukuliwa na chanzo cha habari hii.

Wakati huohuo, mzambia George Lwandamina amesema hajasaini mkataba wowote na Yanga ingawa amekiri Yanga inamuhitaji.

Amesema kwamba, kama watakubaliana yupo tayari kuja na kuipa Yanga mafanikio zaidi.

Thursday, October 13, 2016

WATANZANIA WAINGIA LIGI KUU YA SWEDEN

Baada ya kupanda daraja Sweden, Kilimanjaro FC kusajili Watanzania

BAADA ya kufanikiwa kupanda daraja, kutoka ligi daraja la saba hadi daraja la sita, Kilimanjaro FC-timu iliyoanzishwa na Watanzania nchini Sweden inakusudia kuongeza nguvu katika kikosi chao kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi daraja la 6 nchini humo.

Timu hiyo imeanzishwa kwa lengo la kuwasaidia wanasoka wa Afrika Mashariki siku zijazo kucheza soka barani Ulaya.


“Mikakati yetu ni kujiimarisha zaidi ili ikifika mwezi April mwaka ujao ligi itakapoanza tufanye vizuri zaidi ya ilivyokuwa katika ligi daraja la saba. Malengo yetu ni kutoka daraja la sita twende ligi daraja la tano,” anasema mchezaji wa timu hiyo, Shekhan Rashid nilipofanya naye mahojiano akiwa nchini Sweden.

“Tumejipanga kufanya maandalizi mapema, maana kila kitu kipo sawa, zaidi tunaomba Mungu tu atujalie atujalie uzima. Tutaangalia uwezekano wa kuongeza baadhi ya wachezaji kama watatu ambao ni Watanzania wako hapa Sweden ila hawakuwa na usajili. “

“Usajili wao utatuimarisha maana sasa ni ngumu kusajili mchezaji kutoka Tanzania, sheria hairuhusu. Kuanzi ligi daraja la 3 hadi ligi kuu ndiyo tunaweza kuleta wachezaji kutoka nje,” anasema Shekhan mchezaji wa zamani wa Simba SC, Mtibwa Sugar, Moro United na Azam FC za hapa Tanzania.

“Tunawaomba Watanzania waendelee kutusapoti na tunawashukuru sana kwa sapoti yao maana hii timu malengo yetu ni kuja kuwawekea njia wadogo zetu kurahisha wapate nafasi ya kucheza huku.”
“Kama nilivyokwambia, tukifika kuanzia daraja la tatu tunaruhusiwa kuleta wachezaji kutoka Tanzania kwani tutakuwa katika ligi za kulipwa na itakuwa faida kubwa sana kwa timu yetu ya Taifa.”

“Hakuna kingine, tunafanya hivi kusaidia Watanzania wenzetu. Furaha yangu na wenzangu waliopo huku ni kuja kuona watu wanafaidika na matunda yetu. Mungu atatusimamia kwa hili.”

Wednesday, October 5, 2016

Break News! TFF yatoa adhabu kwa Simba kutokana na uharibifu wa uwanja wa taifa




Kamati ya bodi ya ligi ya uendeshaji imetoa adhabu kwa vilabu kadhaa kufutia vilabu hivyo kukutwa na makosa mbalimbali.



Kubwa zaidi na lililokuwa likisubiriwa ni kuona hatua gani zitachukuliwa kwa klabu ya Simba kufuatia mashabiki wake kung’oa viti wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Yanga uliochewa October Mosi kwenye uwanja wa taifa.

Simba imetozwa faini ya shilingi 5,000,000 (milioni tano) pamoja na kulipa gharama za uharibifu wa viti uliofanywa na mashabiki wa klabu hiyo.


Soma taarifa rasmi iliyotolewa na TFF kuhusu adhabu mbalimbali zilizotolewa kwa vilabu vilivyokutwa na hatia katia makosa ambayo vilikuwa vikituhumiwa nayo.

ZFA yaikaribisha Yanga Zanzibar baada ya kuomba uwanja wa Amaan




Chama cha Soka visiwani Zanzibar ‘ZFA’ kimepokea kwa mikono miwili taarifa za klabu ya Yanga kumuandikia barua Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Zanzibar kuomba kuutumia uwanja wa Amaan kwa mashindano mbalimbali ambayo inashiriki ikiwemo ligi kuu Tanzania bara pamoja na mashindano mengine.
Afisa Habari wa ZFA Ali Bakar ‘Cheupe’ amethibitisha kuiona barua hiyo kupitia mitandao mbali mbali ambapo amesema wao kama ZFA hawana matatizo yoyote na wapo tayari hata baadhi ya michezo ya Ligi kuu Zanzibar kuisogeza hadi saa 12 jioni kuipisha Yanga au Yanga kucheza 12 jioni kupisha ligi kuu ya Zanzibar.
Amesema endapo Yanga wakikubaliwa kuutumia uwanja huo wa Amaa,  ZFA inaikaribisha Yanga visiwani Zanzibar.
“Tumeziona taarifa hizo kupitia mitandao mbali mbali, sisi ZFA tunathibitisha barua hiyo tumeiona, na  sisi kama chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar hatuna pingamizi juu ya klabu ya Yanga ambao ni sehemu ya Jamhuri ya Tanzania, sisi tunawambia karibu Zanzibar na tupo pamoja ikiwa watapata ridhaa huko walipoomba,” alisema Cheupe.

Barua hiyo ya Yanga iliyoandikwa na Katibu wao Baraka Deuedit imetumwa moja kwa moja kwa Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Zanzibar huku nakala ikienda kwa Chama cha Soka Visiwani Zanzibar ‘ZFA’.

ETHIOPIA YAFUTA MCHEZO DHIDI YA TAIFA STARS




Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepokea barua kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Ethiopia (EFF), ikielezea juu ya kufutwa kwa mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliokuwa ufanyike Oktoba 8, 2016.
EFF imesema kwamba imelazimika kufuta mchezo huo ulikuwa kwenye kalenda ya FIFA kwa sababu za hali ya hewa si rafiki kwa sasa nchini Ethiopia.

Kwa barua hiyo, Kocha Mkuu wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania (Taifa Stars), Charles Boniface Mkwasa atalazimika kuvunja kambi ya timu hiyo ambayo iliweka kwenye Hoteli ya Blue Pear iliyoko Ubungo, Dar es Salaam.
Mchezo huo uliratibiwa kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ambalo huwa na kalenda ya wiki ya mechi za kimataifa kwa wanachama wake – Tanzania ni miongoni mwao. EFF, ndio walioomba nafasi hiyo.
Ingekuwa ni faida kwa Tanzania kama ingeshinda mchezo huo kwa maana kina alama za nyongeza kama inatokea unaifunga timu mwenyeji.
Matokeo yake yangekuwa ni sehemu malumu kupima viwango vya ubora na uwezo wa timu za taifa. Kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya 132 kati ya nchi 205 wanachama wa FIFA zilizopimwa ubora. Ethiopia yenyewe inashika nafasi ya 126.
Argentina inaongoza ikifuatiwa na Ubelgiji anakocheza Mbwana Samatta – nyota wa kimataifa wa Tanzania. Samatta anacheza klabu ya K.R.C Genk inayoshiriki Ligi Kuu ya Ubelgiji. Timu nyingine bora kimataifa ni Ujerumani, Colombia na Brazil.

Katika Bara la Afrika, Ivory Coast ambayo ni ya 34 kwa ubora duniani ndiyo inayoongoza ikifuatiwa na Algeria, Senegal, Tunisia na Ghana

Sunday, September 25, 2016

TAIFA STARS KUJIPIMA NA ETHIOPIA




Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania (Taifa Stars), inatarajiwa kucheza na Ethiopia katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa Oktoba 8, 2016.

Mchezo huo utakaofanyika jijini Addis Ababa, umeratibiwa kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ambalo huwa na kalenda ya wiki ya mechi za kimataifa kwa wanachama wake – Tanzania ni miongoni mwao. Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ethiopia (EFF), wameomba mchezo huo ufanyike kwao.

Hii ni faida kwa Tanzania kama itashinda mchezo huo kwa maana kina alama za nyongeza kama inatokea unaifunga timu mwenyeji.

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa atakuwa na nafasi ya kuandaa kikosi chake kuanzia Oktoba 3, 2016 mara baada ya michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambako Mwadui itacheza na Azam huku Mbao ikishindina na JKT Ruvu Oktoba 2, mwaka huu kabla ya kupisha kalenda hiyo ya FIFA ya michuano ya kimataifa.

Matokeo ya mchezo huo, ni sehemu malumu kupima viwango vya ubora na uwezo wa timu za taifa. Kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya 132 kati ya nchi 205 wanachama wa FIFA zilizopimwa ubora. Ethiopia yenyewe inashika nafasi ya 126.

Argentina inaongoza ikifuatiwa na Ubelgiji anakocheza Mbwana Samatta – nyota wa kimataifa wa Tanzania. Samatta anacheza klabu ya K.R.C Genk inayoshiriki Ligi Kuu ya Ubelgiji. Timu nyingine bora kimataifa ni Ujerumani, Colombia na Brazil.

Katika Bara la Afrika, Ivory Coast ambayo ni ya 34 kwa ubora duniani ndiyo inayoongoza ikifuatiwa na Algeria, Senegal, Tunisia na Ghana.

SIMBA, YOUNG AFRICAN WAPEWA SIKU TATU TU......




Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za wachezaji imetoa siku tatu kuanzia jana Septemba 24, 2016 kwa viongozi wa klabu za Simba SC na Young Africans SC kukaa chini na kumaliza suala la usajili wa mchezaji Hassan Ramadhani Kessy kwa njia ya mazungumzo ya kuelewana.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya mjadala wa muda mrefu kuhusu kesi mbili zilizofunguliwa na Simba mbele ya kamati hiyo inayoongozwa na Mwanasheria Richard Sinamtwa. Kesi ya kwanza iliyofunguliwa na Simba SC ni dhidi ya Young Africans kudaiwa kuingia mkataba na mchezaji Hassan Kessy wakati bado ana mkataba na Simba SC.

Kesi ya pili ni Simba SC dhidi ya mchezaji Hassan Ramadhani Kessy kudaiwa kuanza kufanya mazoezi pia kusajili Young Africans na kwenda nje ya nchi wakati akiwa ndani ya mkataba na Simba SC. Kama hawatafikia mwafaka katika siku tatu walizopewa, mashauri hayo yatarudi mbele ya kamati na kufanya uamuzi kwa mujibu wataratibu, kanuni na sheria zinazoongoza mpira wa miguu Tanzania. Kupitia madai hayo, Simba inataka kulipwa dola 600,000 za Marekani.


Wakati huo huo, kamati imeondoa kifungo cha mwaka mmoja kwa mchezaji George Mpole wa Majimaji ya Songea baada ya klabu hiyo yenye maskani yake Mkoa wa Ruvuma kufikia mwafaka Kimondo FC.

 Pia kamati iliridhia mchezaji Enyina Darlington kutoka Nigeria kuanza kuitumika klabu yake baada ya kukamilisha vibali vya ukazi na kufanya kazi nchini vinavyotolewa na Idara ya Uhamiaji nchini katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Saturday, September 24, 2016

ARSENAL KUVUNJA MWIKO WA MUDA MREFU DHIDI YA CHALSE LEO



Arsenal leo wako nyumbani wakiwa na mtihani mzito watakapokuwa wakiwakaribisha mahasimu wao wa jiji la London Chelsea katika mchezo wa EPL utakaofanyika kunako Uwanja wa Emirates saa 1:30 usiku kwa majira ya Afrika Mashariki.

Arsenal wanaingia katika mchezo huu wakiwa na imani kubwa kutokana na kuwa na kikosi imara msimu kunzia upande wa safu ya ulinzi mpaka ushambuliaji ukilinganisha na misimu kadhaa iliyopita.

Taarifa muhimu kwa kila timu
Mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud leo anaweza kurejea baada ya kukosekana katika michezo miwli iliyopita kutokana na kusmbuliwa na majeraha.

Hata hivyo kiungo Aaron Ramsey bado ataendelea kuwa nje akiunguza jeraha lake la misuli ya paja na kukadiriwa kurudi takriban wiki tatu zijazo.

Kwa upande wa Chelsea, nahodha wao John Terry ataendelea kukosa mchezo wa leo ambao ni mchezo wa tatu mfululizo kufuatia kuendelea na tiba ya jeraha lake la mguu.

Beki mwenzake Mfaransa Kurt Zouma bado ataendelea kubaki nje licha kuwa tayari ameanza mazoezi madogo-madogo.
Kauli za makocha wa timu zote mbili
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger juu ya nidhamu kwa timu yake: “Tumeongea kuhusu hilo kwasababu katika michezo miwili iliyopita dhidi ya Chelsea tumecheza tukiwa pungufu.”

“Hivyo mchezo wa leo utakuwa muhimu sana kwetu kupata matokeo, lakini muhimu zaidi kucheza kwa nidhamu kubwa.”
Kocha wa Chelsea Antonio Conte: “Huu ni mchezo mkubwa sana unawakutanisha mahasimu wakubwa. Ni muhimu zaidi kucheza soka safi.

“Zaidi ya hapo baada ya kufungwa na Liverpool kulitufedhehesha. Lakini leo itabidi tupambane sana maana tunafahamu kuwa tunacheza na si tu timu kubwa bali mahasimu wakubwa.”
Dondoo muhimu za mchezo
Head-to-head
  • Chelsea hawajapoteza mechi tisa zilizopita za Premier League dhidi ya Arsenal (wameshinda mara sita, droo mara 3).
  • Chelsea hawajapoteza mchezo wowote kati ya mitano ya mwisho waliyocheza katika Uwanja wa Emirates (ushindi mara 2, droo mara 3) tangu mara ya mwisho walivyofungwa 3-1 Desemba 2010. Na wameruhusu goli moja tu katika michezo yote hiyo.
  • Arsenal wameshinda kupata goli mbele ya Chelsea kwenye mechi sita zilizopita.
  • Katika mechi tano za mwisho dhidi ya Chelsea, jumla ya wachezaji wanne wa Arsenal wamejikuta wakitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Arsenal
  • Arsenal wanajiandaa kupata ushindi wao wa nne mfululizo kwenye Premier League kwa mara ya kwanza tangu Oktoba mwaka 2015 walivyoweka rekodi ya kushinda mechi tano mfululizo.
  • Arsenal wamepoteza mchezo mmoja tu kati ya 15 iliyopita (wameshinda mara 8, droo mara nne).
  • Alexis Sanchez ameshindwa kufunga hata goli moja kwenye michezo minne ya ligi akiwa kwenye Uwanja wa Emirates.
Chelsea
  • Kocha wa Chelsea Antonio Conte anaweza kucheza michezo mitatu bila ya ushindi kwa mara ya kwanza tangu mara ya mwisho walivyopata sare nne mfululizo wakati akiwa Juventus Macih 2012.
  • Conte hajawahi kupoteza michezo ya ligi mfululizo tangu Desemba 2009 wakati akiwa Atlanta.
  • Chelsea wamepata clean sheet moja tu kwenye michezo yao ya ligi 12 iliyopita, huku wakiruhusu bao kwenye kila mchezo kati ya michezo sita iliyopita ya ugenini.

  • Diego Costa amefunga magoli matano kwenye michezo mitano ya Premier League msimu huu, akifunga kwenye kila mchezo kati ya mitatu iliyopita.
Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com