Featured
Showing posts with label Local News. Show all posts
Showing posts with label Local News. Show all posts

Sunday, August 28, 2016

Serikali yaagiza Mabasi Mapya 165 ya Mwendokasi.Fahamu zaidi hapa.


Serikali imeanza mchakato wa kuagiza mabasi mapya 165 ya mwendokasi yatakayotoa huduma za usafiri kwa wakazi Dar es Salaam kwenye maeneo yasiyo na huduma hiyo.
Tayari imeshatangaza zabuni ya kununua mabasi hayo na mwezi Desemba, mwaka huu itasaini mkataba na mzabuni.

Mtendaji Mkuu wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi (Dart), Ronald Rwakatare amewaeleza wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa waliotembelea mradi huo kuwa wanatarajia mabasi hayo yataanza kazi Aprili mwakani.

“Mabasi haya yatahudumia maeneo ya Morocco, Tegeta, Masaki, Makumbusho na mengine yasiyofikiwa, wakati tukiendelea na ujenzi wa awamu ya pili ya mradi huo,” amesema.

Monday, August 22, 2016

Tanzania Kujenga Kiwanda cha kusindika gesi kugharimu trilion 65



Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 22 Agosti, 2016 amepokea taarifa ya maendeleo ya mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha kusindika gesi asili (LNG Plant) kinachotarajiwa kujengwa katika eneo la Likon'go, Mchinga Mkoani Lindi.
Mwakilishi Mkazi wa Kampuni ya Statoil ya nchini Norway ambayo ni moja ya Kampuni zitakazowekeza katika mradi huo Bw. Oystein Michelsen amemueleza Rais Magufuli kuwa ujenzi wa kiwanda hicho unatarajiwa kugharimu Dola za Kimarekani Bilioni 30 sawa na zaidi ya Shilingi Trilion 65 za Kitanzania na kwamba uzalishaji unatarajiwa kuchukua muda wa zaidi ya miaka 40 baada ya kuanza.
Bw. Oystein Michelsen amebainisha kuwa Serikali ya Norway ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa manufaa ya pande zote na ameomba Serikali ya Tanzania iendelee kutoa ushirikiano ili kufanikisha ujenzi wa kiwanda hicho.
Kwa upande wake Rais Magufuli amemuhakikishia Mwakilishi huyo wa kampuni ya Statoil kuwa Serikali ya Tanzania ipo tayari kuhakikisha mradi unafanikiwa na ameitaka Wizara ya Nishati na Madini kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) kushirikiana na wadau kutoka Wizara nyingine kuharakisha mchakato wa kuanza kwa ujenzi wa kiwanda hicho.
"Nataka kuona mradi huu unaanza kujengwa, tunachukua muda mrefu mno, kamilisheni mambo yaliyobaki ili wawekezaji waanze kazi mara moja" Amesema Rais Magufuli.
Dkt. Magufuli amesema mradi huo unatarajiwa kuzalisha ajira kwa idadi kubwa ya watanzania na utaiwezesha serikali kupata mapato kupitia tozo mbalimbali, na hivyo kutumika kuimaisha huduma za kijamii zikiwemo elimu, afya, maji na miundombinu.
Pamoja na Statoil kampuni nyingine zinazoshiriki katika uwekezaji wa mradi huu ni Shell, Exxon Mobil, Pavillion na Ophir

BREAKING NEWS UVCCM watangaza maandamano nchi nzima




Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) nao umesema unatarajia kufanya "maandamano ya amani" nchi nzima Agosti 31 kwa ajili ya kueleza utendaji kazi bora wa Rais Dkt. John Magufuli kwa watanzania.

Wakati Jeshi la Polisi nchini likiwa limepiga marufuku maandamano ya nchi nzima yaliyotangazwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hii leo Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) nao umesema unatarajia kufanya "maandamano ya amani" nchi nzima Agosti 31 kwa ajili ya kueleza utendaji kazi bora wa Rais Dkt. John Magufuli kwa watanzania.

Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja huo, Shaka Hamdu Shaka amesema tayari wameshamwandikia barua Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa ajili ya kupata kibali cha maandamano hayo na ulinzi huku akiwaeleza wandishi wa habari kuwa kiu yao ni kufikisha ujumbe kwa wananchi juu ya utendaji wa Rais Dk. Magufuli katika kushamirisha dhana ya maendeleo na kuleta mageuzi ya kiuchumi.
Maandamano hayo yataanzia katika ngazi za wilaya yataanzia kwenye ofisi za UVCCM ngazi ya

wilaya na mkoa na kuishia katika ofisi za wakuu wa wilaya na mikoa huku wanachana wa vyama vingine na wapenda maendeleo wakikaribishwa kujiunga na maandamano hayo ya amani.

Profesa Lipumba Aipasua CUF.......Wajumbe Warushiana Viti na Kutukanana, Mkutano Wavunjika





Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Wananchi (CUF), uliofanyika jana jijini Dar es Salaam ukilenga kuwachagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho ulivunjika baada ya wajumbe kuanza kurushiana viti na matusi baada ya kupishana katika hoja ya kumtosa aliyekuwa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba.

Profesa Lipumba alijiuzulu nafasi yake kabla ya kampeni za uchaguzi Mkuu mwaka jana akieleza kuwa roho inamsuta kumnadi mgombea urais aliyeungwa mkono na vyama vya Ukawa. Lakini mwaka huu alirejea na kuandika barua akiomba kurejea kwenye nafasi yake hali iliyozua sintofahamu.

Taarifa kutoka ndani ya Mkutano huo zimeeleza kuwa wajumbe 832 walihudhuria lakini hoja ya kumjadili Profesa Lipumba ilipofikiwa, baadhi ya wajumbe ambao wanamuunga Mwenyekiti huyo wa zamani walizua vurugu wakipinga utaratibu uliotumika.

Baadhi ya wajumbe hao waliwaambia waandishi wa habari kuwa viongozi waliopo madarakani walifanya ubabe kwa kulazimisha kura ya kukubali au kukataa ombi la Lipumba ipigwe kwa uwazi na sio siri kama Katiba inavyoeleza.

“Haki haikutendeka, ni ubabe. Wala mkutano haikuzingatia kutimia kwa akidi. Tulilazimishwa kupiga kura kwa kunyoosha mikono wakati mazingira yaliyopo na usahihi, kura ni siri,” mmoja wa wajumbe hao alikaririwa.

Baada ya kupiga kura za wazi, Lipumba alipata kura 14 kati ya kura 832 hivyo kuonekana kukataliwa kwa kishindo, lakini vurugu zilizuka ghafla kutokana na maamuzi hayo na mkutano ukashindwa kufanikisha zoezi zima la kuwapata viongozi hao wapya.

Katika hatua nyingine, Juma Haji Duni alijiengeu katika kinyang’anyiro cha uchaguzi huo, baada ya baadhi ya wajumbe kusisitiza kuwa katiba inamtaka mtu aliyejiuzulu na kuhamia chama kingine kusubiri miaka miwili ili agombee nafasi ya uongozi ndani ya chama pale atakaporejea.

Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mipango wa CUF, Shaweji Mketo, alisema kuwa Duni alijiondoa kutokana na maadui wa Ukawa kutaka kukihujumu chama hicho.

Mkutano huo umeahirishwa hadi utakapotangazwa tena. 

Afrika Mashariki yatakiwa kuboresha sheria kwenye sekta ya uchimbaji madini





 Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki EADB imezitaka nchi za kanda hiyo kuboresha sheria kwenye sekta ya uchimbaji madini ili kuhakikisha rasilimali zinapangwa kwa usawa.
Akiongea kwenye semina ya kikanda ya majaji kutoka nchi za Afrika Mashariki iliyomalizika jana Nairobi, Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo, Vivienne Yeda, amesema ugunduzi na uchuguzi unaoendelea wa madini katika kanda hiyo umeongeza matumaini ya kuongeza utajiri, kupunguza nakisi ya bajeti na kuboresha maisha ya watu wa nchi hizo. Amesisitiza kuwa mafao lazima yaende kwenye jamii za nchi husika, kwa njia za mirahaba, kodi, mgao, fursa za biashara, kazi za kitaalamu na ajira kwa wafanyakazi wenye ujuzi.
Semina hiyo iliyoandaliwa na EADB, imewalenga majaji wa Afrika mashariki wanaohusika na kazi ya usuluhishaji na kutatua migogoro kwenye sekta ya madini.

USAIN BOLT NA SAKATA LA MAPENZI NA MTOTO WA SHULE




 Picha za bingwa wa mbio za mita 100,200 na relay kwenye mashindano matatu ya Olimpiki Usain Bolt zimeenea kwenye mitandao ya kijamii.
Bolt anaonekana kwenye pozi za mapenzi na msichana anaedaiwa kuitwa Jady Duarte wa umri wa miaka 20 ambae ni mwanafunzo wa chuo kimoja cha Brazil
Inasemakana Bolt alikua tayari kashatangaza kumuoa mchumba wake Kasi Benestt baada ya olimpiki na huenda ndoa hiyo ikaingia doa.
Hata hivyo taarifa hizi huenda zisimtatize sana Bolt kwani yeye amewahi kukubali kwamba hawezi kuwa na uhusiano na mwanamke mmoja.

WEMA ATOA MACHOZI NA KUMUOMBA IDRIS ARUDI




Siku chache baada ya Wema Sepetu na Idriss kutofautiana na Idris kumuondokea Wema,Mwanadada huyo ameonekana kupata tabu sana na maisha bila mpenzi wake.
Hivi kaamua kutumia mtnadao wa kijamii kumuomba msamaha.
Amesema " That moment you realise how much u miss a special someone… Rudi basi… hata kidogo tu

Thursday, August 18, 2016

Sasa Imetosha Kuwa na dada na kaka poa Kinondoni




Licha ya Serikali kuanzisha vita dhidi ya biashara haramu ya uuzaji mwili, Wilaya ya Kinondoni inakabiliwa na ongezeko la biashara haramu ya ngono kwa muda mrefu ambapo eneo la Tandale linatajwa kukithiri vibanda vingi vya dada na kaka poa.
Wakuu wa wilaya wengi wamepita katika wilaya ya Kinondoni pasipo kutokomeza changamoto hiyo. Lakini Mkuu wa sasa wa Wilaya hiyo Mh. Ally Hapi amejidhatiti kuuvunja mwiko huo. Hivi karibuni Hapi alitaja mikakati ya kutokomeza mtandao wa biashara hiyo.
Alisema atahakikisha anavunja vibanda vyote vinavyotumiwa na dada pamoja na Kala poa , vilevile watakaokamatwa watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Hapi alisema amepokea idadi ya vibanda vinavyotumiwa na dada poa na kwamba mpango wake ni kuvifunga kisha kutafuta wawekezaji ili Wamiliki wa vibanda hivyo walipwe fidia na kupisha ujenzi wa vitega uchumi.
“Niliwaagiza watendaji wa kata kuniletea idadi ya madanguro, nimeshajua mahali yalipo madanguro hayo, na kwamba nitakwenda kuchukua hatua ya kufunga madanguro pamoja na kuwapeleka dada poa mahakamani,” alisema. Alisema hatawachukulia hatua za kisheria dada/kaka poa pekee, bali hata wamiliki wa baa zitakazowahifadhi watu hao watachukuliwa hatua.
“Hatutashughulika na dada poa pekee bali hata Wamiliki wa nyumba na au baa watachukukiwa hatua. Hilo likitekelezwa
Kila mtu atatimiza wajibu wake, nimegundua wamiliki wengi wa madanguro hawapo hapa na idadi ya madanguro katika eneo la Tandale pekee kuna vibanda 58.” alisema.

Alisema utekelezaji wa ubomoaji nyumba umeshaanza kujadiliwa na kwamba wanasubiriwa wawekezaji ili wapewe fursa za kujenga maduka na vitega uchumi.
“Tunataka wenye fedha zao waje wawekeze ili tuwalipe fidia wenye nyumba, zibomolewe,” alisema na kuongeza.
“Huu mfupa uliwashinda watangulizi wangu lakini mimi nitautafuna.”
Kuhusu baa zinazokiuka sheria, alisema atawaondoa watendaji wa kata waliokaa muda mrefu kwa sababu wengi wao ndiyo chanzo cha ukiukwaji wa sheria.

“Watendaji waliokaa muda mrefu waondolewe sababu tumegundua hushirikiana na wenye baa kupiga kelele, wanachukua fedha zao na kuwaacha kupiga kelele usiku wa manane kinyume cha tarabibu,”

Mkuu wa Wilaya Kinondoni awapiga ‘STOP’ mgambo kuwafanyia fujo wafanyabiashara wadogo




Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi amewapiga marufuku mgambo wa wilaya hiyo kuwafanyia fujo wafanyabiashara wadogo wanaofanya shughuli zao katika maeneo rasmi.
Hapi aliyasema hayo jana katika kipindi cha Mada Moto kinachorushwa moja kwa moja na kituo cha Channel Ten.
Alisema kumekuwepo na tabia ya baadhi ya watu kuwatoza ushuru kinyume cha sheria wafanyabiashara hao wanaofahamika kwa jina la wamachinga jambo linalosababisha halmashauri ya manispaa ya kinondoni kupoteza mapato.
“Kuna mtu mmoja alikuwa anatoza wamachinga ela, zaidi ya sh 8,000 kwa siku na walikuwa wanalipa, kama serikali ikiweka mfumo mzuri inaweza kupata mapato ya uhakika kutoka kwa wamachinga,” alisema.
Alisema atahakikisha anapata idadi ya wamachinga wote katika wilaya hiyo ili kuwawezesha kiuchumi ikiwemo kuwapa mikopo na kutenga siku ya gulio ili wapate fursa ya kufanya biashara.
“Machinga wote tuwatambue tuwaunganishe na bima ya afya, wapewe mikopo hakika watainuka sababu hakuna mtu aliyezaliwa kuwa machinga muda wote, tunataka Kuwainua ili waje kuwa wafanyabiashara baadae,” alisema.
“Ni marufuku kupiga na kuwasumbua wamachinga, kuwaibia bidhaa zao ni marufuku,” alisema.
“Sisi viongozi kazi yetu ni kuwaongoza na kuwaonyesha Mahala panapostahili wao kufanyakazi, na wilaya yangu ya kinondoni ina mkakati wa kuandaa magulio ili wafanyabiashara ndogondogo wauze bidhaa zao, ” alisema.
Aliongeza kuwa “Nyuma kulikuwa na mianya ya upotevu wa mapato, tumefanya kazi kubwa Na kamati ya usalama na sasa watu wanafurika kulipa kodi. “

“Tunawaomba watanzania watuombee kwa kuwa tunaopambana nao siyo wote wanafurahi. Wananchi washiriki katika kutoa taarifa za wakwepa kodi na kadhalika,” alisema.

kijana wa miaka 16 anayetumia akili ya ziada kutengeneza pesa nyingi




Mwanafunzi wa Chuo Robert Mfune mwenye umri wa miaka 19, ameweza kutengeneza zaidi ya maelfu ya Paundi za Uingereza akiwa anafanyakazi katika muda wa ziada kwenye mgahawa ya McDonald’s kama mhudumu.
Robert ambae alipokua na umri wa miaka 16 tu, alianza kufanya kazi kama mhudumu katika kampuni ya McDonalds nyumbani kwao Southampton, ambako alipata kujifunza mambo mengi kuhusu biashara, na baadae kuanza kufanya biashara zake mwenyewe na kuweza kutengeneza pesa za kutosha kununua gari ya kifahari aina ya Bentley na kumnunulia nyumba ya kuishi mama yake mzazi.
Alisema ilikua ngumu sana kwake kufanya kazi katika mgahawa ya McDonald’s, kufanya biashara zake na kusoma kwa wakati mmoja.
“Nikama kwenda chuo na hela ya mkopo, kama utazingatia masomo na kuweka malengo ya kufanya vizuri basi utafanikiwa”. alisema mfanyabiashara Mfune. 
Mafanikio yake yalianza baada ya kumaliza masomo yake ya chuo, na kufanya kazi kama mhasibu katika idara ya fedha. Hivyo kumpelekea kupata ujuzi zaidi katika mambo ya biashara, na kuanza kufanya biashara zake akitumia akaunti zenye jina la mama yake na kuweza kupata mafanikio hayo.
“Nilipokua mhudumu nilijitahidi kujifunza mambo kazaa hivyo nikienda nyumbani nafanya utafiti mwenye na kufanya cha kwangu”. alisema Mfune.
Mfune kwa sasa anafanya biashara zake kwa kutumia akaunti yake mwenyewe, huku pia akiwa ameweza kuwekeza katika Migahawa ya chai mbalimbali mjini Uingereza.

Pia anamiliki magari yenye thamani ya zaidi ya Pauni 250,000£ ikiwemo Range Rover, Bentley continental GT ya rangi ya dhahabu lakini amedai kwamba yeye sio mtu wa kuthamini mali na magari bali utu wa watu na kujali marafiki zake.


Friday, August 12, 2016

Gazeti la Mseto nje kwa miaka 3




Serikali nchini Tanzania imelifungia gazeti la kila wiki la Mseto kuchapishwa katika njia zote ikiwa ni pamoja na mitandao. Hili ni gazeti la pili kufungiwa ndani ya mwaka mmoja.
Serikali inasema Mseto limekuwa likiandika taarifa za uongo na kugushi kwa kutumia nyaraka mbalimbali za serikali huku taarifa hizo zikiwa na nia ya uchochezi na kumchafua Rais John Magufuli na viongozi wengine wa serikali yake.
Akitangaza kufungiwa kwa gazeti hili mapema leo hii, Waziri mwenye dhamana ya habari Nape Nnauye amewaambia waandishi wa habari kuwa amelifungia gazeti hilo kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976
Hakuna taarifa rasmi yoyote ya mwitikio wa kufungiwa huko kutoka kwa wachapishaji na wamiliki wa gazeti hilo
Hili ni gazeti la pili kufungiwa ndani ya mwaka mmoja. Mwezi Januari mwaka huu, serikali ililifungia pia gazeti la Mawio muda wote.
Wasiwasi miongoni mwa wadau wa habari umeendelea kuongezeka kwa kile kinachoonekana kuwa utawala huu mpya unaviminya vyombo vya habari na kukandamiza uhuru wa kutoa na kupokea habari pia hapa nchini Tanzania.
Tayari watu wawili wameshtakiwa baada ya kuandika jumbe katika mitandao ya kijamii zilizoonekana kumtusi Rais Magufuli
Inawezekana kufungwa huku kwa gazeti la Mseto kutaibua ukosoaji hasa kutoka kwa wanaharakati wa haki za binadamu ambao wamekuwa wakiikosoa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 ambayo wanasema inatoa mamlaka makubwa sana kwa serikali kuminya uhuru wa habari nchini 

Wafahamu vijana 10 wa chini ya miaka 30 walio matajiri zaidi duniani




Tajiri mmiliki wa ardhi ambaye pia amekuwa akisaidia wasiojiweza katika jamii, Mtawala wa Westminister Gerald Cavendish Grosvenor amefariki na kumwachia mwanawe Hugh Grosvenor urithi wa £9bn.
Alikuwa na binti watatu, na mwana mmoja pekee wa kiume, Hugh, mwenye umri wa miaka 25.
Hugh amerithi "nusu ya London" kwani ardhi nyingi maeneo mengi ya Belgravia na Mayfair, London ilimilikiwa na babake.
Yeye hufanya kazi katika kampuni ya Bio-bean, kampuni inayoangazia teknolojia isiyoongeza gesi zinazochangia ongezeko la joto duniani.
Kwa mujibu wa orodha ya jarida la Forbes ya mwaka 2016, kuna vijana wengine tisa wa chini ya umri wa miaka 30 ambao utajiri wao ni zaidi ya dola bilioni moja za Marekani.
Vijana wengine matajiri ni:
2 & 3: Alexandra, 20, na Katharina Andresen, 21
Ndio wachanga zaidi na wanamiliki kampuni ya Ferd.
Binti hawa walirithi utajiri hu kutoka kwa baba yao Johan, raia wa Norway mwaka 2007.
4: Gustav Magnar Witzoe, 23
Anatoka Norway pia na huonesha maisha yake ya kifahari kwenye Instagram.
Amerithi sehemu ya biashara ya babake ya kufuga samaki na sasa utajiri wake ni $1.1bn (£846m).
Gustav Witzoe, babake ambaye wana jina sawa, alimpa hisa kwenye kampuni hiyo kama zawadi. Lakini hana udhibiti au usemi wowote.
5&6: Ludwig Theodor Braun na dadake
Haonekani sana mtandaoni. Hayupo kwenye Twitter au Instagram lakini anatambuliwa kwa utajiri.
Familia yake ilianzisha kampuni ya dawa ya B. Braun Melsungen, Ujerumani 1839.
Kampuni hiyo ni maarufu sana kwa dawa na vifaa vya matibabu.
Ludwig humiliki 10% ya kampuni hiyo ambayo ni sawa na $1.8bn (£1.4bn).
Dadake Eva Maria Braun-Luedicke yuko nyuma yake kidogo lakini utajiri wake ni $1.4bn (£1bn).

7&8: Waanzilishi wa Snapchat


Image copyright Getty Images
Image caption Waanzilishi wa Snapchat Evan Spiegel na Bobby Murphy
Evan Spiegel ni mmoja wa walioanzisha mtandao wa Snapchat ambao hutumiwa na mamilioni ya vijana duniani.
Majuzi, aliingia uchumba na mwanamitindo mashuhuri duniani Miranda Kerr.

Image copyright Getty Images
Ana umri wa miaka 26 na utajiri wake ni $2.1bn (£1.6bn), Evan ndiye mchanga zaidi miongoni mwa waanzilishi wa Snapchat na ndiye tajiri zaidi miongoni mwao.
Mwenzake ni Bobby Murphy, 28, ambaye anamkaribia sana kwa utajiri.
Utajiri wa Murphy ni $1.8bn (£1.3bn).
9: Lukas Walton
Kwa mujibu wa Forbes, Lukas Walton, 29, ndiye anayemkaribia sana Hugh Grosvenor.
Utajiri wake ni $10.4bn, ambazo ni karibu £7.2bn kwa viwango vya sasa vya ubadilishanaji wa fedha vya sasa.
Anatoka katika familia tajiri inayomiliki Walmart (miongoni mwa kampuni nyingine), ambayo pia humiliki Asda nchini Uingereza.
10: Wang Han
Wang Han, raia wa China, anakamilisha orodha hii.
Chanzo cha utajiri wake ni urithi wa hisa za kampuni ya ndege ya Juneyao Air kutoka kwa babake Wang Junyao, aliyefariki 2004.
Junyao alikuwa mwanzilishi wa kampuni ya Juneyao Group. Wang Han humiliki 27% ya hisa za shirika hilo la ndege na 14% ya hisa za maduka ya jumla ya Wuxi Commercial Mansion Grand Orient.
Utajiri wake unakadiriwa na Forbes kuwa $1.34bn.

Sunday, August 7, 2016

Madawati ya Mbunge Wa Chadema ya Kataliwa Kisa.....





BUNDA, MARA: Madiwani wa CCM katika jimbo la Bunda wamekataa kupokea madawati yaliyotolewa na Mbunge Ester Bulaya wa CHADEMA.
- Inadaiwa wameyakataa sababu yalikuwa yameandikwa majina ya Mbunge huyo.

Saturday, July 30, 2016

Tanzania kujitengeneza ndege aina ya helikopta Kwa Mara Ya Kwanza




Raia nchini Tanzania wameamkia habari za kushangaza kwamba taifa hilo linaunda ndege.
Gazeti la Tanzania la Daily News limeripoti kwamba ndege hiyo aina ya helikopta inakaribia kukamilika na kwamba habari hiyo imekuwa ikisambaa barani Afrika kwa kasi.
Gazeti la Zambia, Observer linasema kuwa lengo la ndege hiyo itayokuwa ikibeba watu kwa bei rahisi itakabiliana na matatizo ya uchukuzi nchini humo.
Huku gazeti la Cameroon, Concord likisema kuwa mradi huo ni wa kihistoria linaongezea kuwa lengo lake ni kutengeza ndege 20 kwa mwaka.
Ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba watu wawili inakaribia kukamilika katika chuo cha ufundi cha Teknolojia cha Arusha na itaanza kufanyiwa majaribio ya kuruka angani baada ya kuruhusiwa na mamlaka ya uchukuzi wa angani nchini Tanzania kulingana na Daily News.



WAZUNGU WAMTEMBELEA MTENGENEZAJI HELIKOPTA TUNDUMA
** Mkazi wa Tunduma, mkoani Songwe, Adam Kinyekile (34) ambaye alikuwa akitengeneza helikopta amepata mwaliko maalumu na wazungu kutoka Afrika Kusini kutembelea kiwanda chao cha kutengeneza chopa.
Kijana Kinyekile ambaye pia ni fundi magari alitumia ubunifu wake kuunda helikopta, kitu ambacho kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, George Mbijima akiwa mjini Tunduma alimtembelea kisha kuweka jiwe la msingi kwenye helikopta hiyo.
Hata hivyo baada ya taarifa za kijana huyo kurushwa kwenye vyombo vya habari , Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) ilipiga marufuku kwa mtu yoyote kutojihusisha na utengenezaji au ubunifu wa ndege bila kufuata taratibu.
Onyo hilo lilionekana kumlenga Kinyekile kwa kazi yake aliyokuwa akiifanya jambo ambalo lilimfanya asiweze kuendelea na maboresho ya helikopta yake licha ya kudai ilikuwa imebaki kuruka.

Huyu Ndege aliyesafiri kutoka Finland hadi Uganda

Ndege mmoja ambaye inaaminika alitoka nchini Finland amepatikana katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda.
Ndege huyo aina ya Osprey kwa sasa anatunzwa na maafisa wa kituo cha kuwahudumia wanyama cha Uganda Wildlife Education Centre (UWEC).


Ndege huyo mkubwa, aina ya mwewe, aligunduliwa na maafisa wa uwanja wa ndege katika njia inayotumiwa na ndege kupaa na kutua katika uwanja wa huo wa Entebbe.
Isaac Mujaasi, afisa wa mauzo na mawasiliano katika UWEC, ameambia BBC kwamba ndege huyo alikuwa ameumia katika mabawa yake baada ya kugongwa na ndege iliyokuwa inapaa.





Alikuwa na pete yenye maelezo kumhusu mguuni ambayo inaashiria kwamba alimilikiwa na makumbusho ya historia asilia nchini Finland.





Bw Mujaasi anasema waliwasiliana na maafisa wa makumbusho hao ambao wamethibitisha kwamba ndege huyo ni wao.


“Hili lilituthibitishia kwamba ndege huyu alisafiri kutoka Helsinki, Finland,” Bw Mujaasi amesema. “Tutamtibu ndege huyo na akipona tutamwachilia na huenda akarejea kwao.”
Afisa huyo hata hivyo amesema ni kawaida kwa ndege kuhama kutoka Ulaya, hasa wakati wa majira ya baridi na kukimbilia maeneo yenye joto.

Thursday, July 28, 2016

Mchina aliyemfanyia unyama Mtanzania atiwa mbaroni.




Waziri wa mambo ya ndani ya nchi,Mwigulu Nchemba hii leo amewasili mkoa wa Geita kwa ziara ya kikazi kubwa ikiwa ni kufuatia taarifa za mateso na mauaji yaliyofanywa na raia wa china wanaomiliki sehemu ya mgodi wa Nyamhuna uliopo Katoro-Geita dhidi ya wafanyakazi/vibarua ambao ni watanzania.
Takribani wiki moja sasa kumekuwa hali ya sintofahamu dhidi ya picha zinazoenezwa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari zikionesha raia wa tanzania anayefanya kazi kwenye mgodi tajwa akiteswa na kufanyiwa vitendo vya kinyama na mwajili wake ambaye ni raia wa china.
Imemlazimu waziri mwenye dhamana na usalama wa raia na mali zao kupitia wizara ya mambo ya ndani kufika eneo la mgodi kujiridhisha kwa taarifa zilizotapakaa na kubeba simanzi kwa watanzania.

Mwigulu Nchemba amejiridhisha kuwa kulikuwepo na tukio hilo la mtanzania kuteswa na huyo mwajili wake kipigo kilichopelekea kupoteza fahamu na sio kifo.
Hatua za awali mwigulu alizozifanya ni kwenda gereza la Geita mjini alikohifadhiwa kijana huyo kwa madai ameshitakiwa na mwajili wake kwa kosa la wizi lililopelekea yeye kupigwa.
Katika mahojiano ya waziri Mwigulu Nchemba na kijana huyo,Mwigulu alibaini kuwa kijana huyo aliyepo gerezani ndiye mhanga wa tukio lile kwa uthibitisho wa makovu yaliyopo mwili mwake na mavazi aliyovalia wakati anateswa na wakati yupo hapo gerezani.
Katika hali hiyo ilimlazimi Mh.Mwigulu kwenda mgodini akiwa ameambatana na kijana huyo kwaajili ya kutambua waliofanya vitendo hivyo vya kinyama.
Katika oparesheni hiyo, kijana aliyeteswa na kujeruhiwa aliwabaini watanzania 5 ambao ni walinzi wa eneo hilo na mchina mmoja walioshirikiana kumpiga,kumtesa na kumjeruhi.


Copyright © 2015 Dar One
| Distributed By Hotrootnews.blogspot.com